|
Anasema
Sheikh Ibn
Uthaymiyn (Mwenyezi
Mungu amrehemu):
Zipo
dalili nyingi
sahihi
zinazoelezea juu
ya Adhabu
ya kaburini.
Mwenyezi Mungu
anasema:
Adhabu
ya Motoni
wanadhihirishiwa (makaburini
mwao) asubuhi
na
jioni .
Na siku ile
kitakapotokea
Kiama (kutasemwa) Waingizeni
watu
wa
Firauni katka
adhabu kali
zaidi.
Al
Muumin (Ghafir
- 46)
Hii
ni dalili
katika Qurani
kuwa Firauni
na watu wake
wanadhihirishiwa
adhabu asubuhi
na jioni kabla
ya Siku
ya Kiama.
Kwa sababu aya
inaendelea kusema : Na
siku ile
kitakapotokea
Kiama na maana
yake ni kuwa
hiyo adhabu
iliyotajwa ya
kudhihirishiwa Moto
asubuhi na
jioni ilikuwepo
kabla ya
Siku ya
Kiama.
Na
katika hadithi
nyingi sahihi
Mtume
wa
Mwenyezi Mungu (SAW)
amesema:
Muombeni
Mwenyezi Mungu
akukingeni
na adhabu
ya Moto.
Wakasema: Tunajikinga
kwa
Mwenyezi Mungu
na adhabu
ya Moto.
Akasema: Muombeni
Mwenyezi Mungu
akukingeni
na adhabu
ya Kaburi.
Wakasema: Tunajikinga
kwa
Mwenyezi Mungu
kutokana na
adhabu ya
Kaburini.
Muslim 2867
Na
Mtume wa
Mwenyezi Mungu
(SAW) pia
alisema juu
ya
Muislamu :
Anapanuliwa
kaburini mwake
kiasi cha upeo
wa macho yake.
Bukhari
1374
Dalili
kama
hizi ziko
nyingi sana,
na haijuzu
mtu kuzikanusha
kwa ajili
ya matamanio
ya nafsi
yake.
Adhabu
ya kaburini
ni
ya kiroho
na si
jambo
linalohusu mwili,
na hii
ndiyo sababu
ikawa imani
juu yake
ni katika
mambo ya ghaibu.
Na hali ya
mambo katika
maisha ya
Barzakh
hayawezi kukisiwa
kwa
hali ya
maisha yetu
ya hapa
duniani.
Isitoshe,
adhabu ya
Kaburini
na neema
zake
anayadiriki maiti
peke yake
na wanadamu
wengine
hawawezi kuyaona
wala kuhisi
au kuyadiriki.
Mfano wake ni
sawa na
mfano wa
mtu anapoota
usingizini.
Anaota
kuwa anakwenda
anarudi,
anapigwa anapiga.
Anajiona yupo
mahali penye
nafasi kubwa
na
mara nyingine
anajiona yupo
penye nafasi
ndogo
iliyodhikika.
Anayaona
yote wakati
walio karibu
yake hawayaoni
wala hawayahisi.
(Mwisho
wa
maneno ya
Sheikh Ibn
Uthaymiyn
Kama
ilivyoeleza aya
ya adhabu
wanayopata
Firauni na
watu wake hadi
siku ya
kiama, pia
zipo aya
nyingi
zinazoelezea juu
ya neema
wanayopata
Waumini na
pia juu
ya adhabu
wanayopata
makafiri wanapotolewa
roho zao,
na baada
ya kutolewa
roho zao.
Mwenyezi
Mungu anasema:
Na laiti
ungeliona
Malaika wanapowafisha wale
waliokufuru
wakiwapiga nyuso
zao
na
migongo yao
na kuwaambia;
Ingojeni adhabu
ya moto.
Hayo
ni
kwa sababu
ya (maasi)
yake
yaliyofanya na
mikono yenu.
Na hakika
Mwenyezi Mungu
si mwenye
kuwadhulunu
waja (waka)
Al Anfal
50-51
Na akasema
juu ya
Mashuhadaa:
Wala
usiwadhani wale
waliouawa katika
njia ya
Mwenyezi Mungu
kuwa
ni wafu
(maiti) bali
wahai
wanaruzukiwa kwa
Mola wao.
Wanafurahia
aliyowapa
Mwenyezi Mungu
kwa
fadhila Zake
na
wanawashangilia wale ambao
hawajajiunga
nao, walio
nyuma yao
ya kwamba
haitokuwa hofu
juu yao
wala
hawatohuzunika.
Aali
Imran -169-170
Aya
kama hizi
za kuadhibishwa
makafiri pale
wanapotolewa roho
zao na
baada yake,
pamoja na
neema
wanazopata Waislamu
wanapotolewa
roho zao
na baada
yake pamoja
na Adhabu
wanayopata
Firauni na
watu wake ni
nyingi sana,
jambo
linalotufanya tusiweze
kukanusha juu
ya adhabu
ya kaburini
zilizotajwa
wazi wazi
na Mtume
wa Mwenyezi
Mungu katika
hadithi zake
nyingi sahihi
tulizozitaja na
tusizozitaja.
Wallahu
taala aalam
Wassalaam
alaykum
wa
Rahmtullahi wa
Barakatuh
|