|
Ndugu Waislam, wakati tunaelekea kukaribia kuuaga mwezi
mtukufu wa Ramadhaan, ambao umejaa fadhila nyingi na kheri
zisizopatikana katika miezi kumi na moja iliyobaki,
kuna
umuhimu mkubwa wa kuendeleza zoezi hili la Funga baada ya
mwezi huu mtukufu hususan, na kwa mwaka mzima kwa ujumla
Insha-Allah.
Swawm kwa ujumla na Swawm za Sunnah haswa ni jambo kubwa
sana la kiibada. Na ni bora sana ieleweke ndugu zangu, kuwa
Swawm si Ibada ifanyikayo katika mwezi wa Ramadhaan pekee,
bali ni jambo ambalo linalofanyika mwaka mzima katika
nyakati mbalimbali kama tutakavyoona katika makala haya.
Kama ilivyo katika Ibada ya Swalah, kuna Swalah za Sunnah au
Rawaatib au Nawaafil, ambazo ndizo zitakazokuwa viraka siku
ya kiyama wakati zile Swalah za Fardh zitakapopelea katika
Mizani. Nazo Swawm za kujitolea au za Sunnah, ndizo
zitakazomuongezea mja thawabu na ujira pamoja na ile Swawm
yake ya Fardh ambayo ni Ramadhaan.
Hapa chini tutaziorodhesha Swawm za SUNNAH ambazo Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
kazipendekeza kwetu tuzitekeleze:
1. SWAWM YA SIKU SITA ZA MWEZI WA SHAWWAAL
Swawm hii inafuatia moja kwa moja baada ya mwezi wa
Ramadhaan na siku ya ‘Iyd ul Fitr. Na Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
anasema:
))
من صام رمضان ثم أتبعه ستاً من شوال كان كصيام الدهر))
رواه مسلم و الترمذي و ابن ماجه , أبو داود و أحمد.
((Atakayefunga mwezi wa Ramadhaan, kisha akafuatia kwa
kufunga siku sita za mwezi wa Shawwaal, basi atapata ujira
wa aliyefunga mwaka mzima)).
Imepokewa na Maimaam Muslim, At Tirmidhy, Ibn Maajah, Abu
Dawuud na Ahmad.
Maulamaa wanachambua sababu ya kulipwa mja ujira wa mwaka
mzima kwa atakayefunga Ramadhaan na siku sita hizo za
Shawwaal, kwa kusema: Jambo zuri hulipwa ujira mara kumi,
kwa hiyo mtu akifunga siku 30 za Ramadhaan atapata ujira
mara kumi; nazo zitakuwa 300, ukijumlisha na siku sita za
Shawwaal ambazo zikilipwa mara kumi, huwa 60. Kwa hivyo
300+60 = 360, mtu atapata hesabu ya mwaka mzima.
Kwa mantiki hii, tunaona kuna umuhimu na ubora mkubwa wa
kuifunga Swawm hii ndugu zangu.
2. SWAWM YA SIKU YA ‘ARAFAH (Kwa wale wasiokwenda kuhiji)
Imesimuliwa na Abu
Qutaadah kuwa Mtume
صلى الله عليه
صلى
الله عليه وآله وسلم
alisema:
عنْ
أَبي قتَادةَ رضِي اللَّه عَنْهُ ، قالَ
:
سئِل رسولُ اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ
وسَلَّم
: عَنْ صَوْمِ يوْمِ عَرَفَةَ ؟ قال
:((
… يكفِّرُ
السَّنَةَ المَاضِيةَ وَالبَاقِيَةَ
((
رواه مسلمٌ
.
Imetoka kwa Abu Qataadah
رضِي اللَّه عَنْهُ
kwamba Aliulizwa Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
kuhusu Swawm ya 'Arafah akasema ((Inafuta madhambi ya mwaka
uliopita na mwaka uliopo))
Muslim
3. SWAWM YA SIKU TATU KATIKA KILA MWEZI ’AYAAMUL BIYDH’
Imesimuliwa na Abu Hurayrah
رضي الله عنه
kwamba Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alisema:
))"من
صام
ثلاثة أيام من كل شهر فذلك صوم الدهر فأنزل الله عز وجل تصديق
ذلك في
كتابه { من جاء بالحسنة فله عشر أمثالها } فاليوم بعشرة أيام))
رواه
الترمذي
قال
الشيخ الألباني : صحيح
((Yeyote atakayefunga kila mwezi siku tatu,ni sawa amefunga
mwaka mzima, kisha Mwenyeezi Mungu akashusha Aya
ithibitishayo maneno ya Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
isemayo: {{Atakayetenda jambo zuri basi malipo yake ni mara
kumi mfano wake}}. Siku moja kwa malipo ya siku kumi!))
Imepokewa At Tirmidhy na kasema
Sheikh
Albaniy kuwa ni Sahihi.
Ukiitazama hadithi hii, utakuta makusudio yaliyotajwa kuwa
malipo ya Funga hiyo ya siku tatu za kila mwezi, ni sawa na
ya mwaka mzima, ni kuwa, ukipiga hesabu ya hizo siku tatu za
kila mwezi, mara miezi kumi na mbili ya mwaka, ni sawa na
siku 36. Na siku hizo 36 mara 10 ambazo ndizo malipo ya kila
siku kwa mara kumi, basi utapata jumla ya
siku
360 ambazo ni takriban idadi ya mwaka mzima wa Kiislam.
Fadhila zilizoje na Ujira mrahisi kiasi gani wa kuuchuma
ndugu watukufu!
Masiku
haya matatu huitwa Masiku Meupe ‘‘Ayaam ul Biydh’’,kwa
ushahidi (mashiko) yafuatayo:
Abu Dharr Al Ghifaari anasimulia kuwa Mtume
صلى
الله عليه وآله وسلم
alimwambia:
))
"يا أبا ذر
إذا صمت من الشهر ثلاثة أيام فصم ثلاث عشرة وأربع عشرة
وخمس عشرة))
رواه
الترمذي قال الشيخ الألباني : حسن صحيح
((Ee Abu Dharr! Endapo utafunga siku tatu za kila mwezi,
basi funga siku ya 13, ya 14, na ya 15))
Hizi huitwa ‘Ayaam ul Biydh’
[Masiku
Meupe]. Imepokewa na At Tirmidhy na kasema Sheikh Albaaniy
kuwa ni Sahihi..
4. SWAWM YA JUMATATU NA ALKHAMIYS
عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: كان رسول الله صلى الله عليه
وسلم يصوم
الإثنين والخميس وعندما سئل قال: (( تُعْرَضُ الْأَعْمَالُ
يَوْمَ
الِاثْنَيْنِ وَالْخَمِيسِ فَأُحِبُّ
أَنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأَنَا
صَائِمٌ }))
رواه الترمذي وقال حديث حسن
Abu Hurayrah
رضي الله عنه
anasimulia kuwa Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alikuwa akifunga Jumatatu na Alkhamiys. Alipoulizwa sababu
ya Swawm katika siku hizo, akajibu: ((Matendo ya Wanaadam
huwekwa mbele ya Mwenyeezi Mungu kila siku ya Jumatatu na
Alkhamiy, nami napenda matendo yangu yawekwe mbele ya Allaah
nikiwa nimefunga)).
Imepokewa At-Tirmidhy na kasema Hadiyth Hassan
5. SWAWM YA SIKU YA TASU’AA NA ‘ASHURAA
Hizi ni Swawm za siku ya tisa na ya kumi ya mwezi wa
Muharram (Mwezi wa kwanza katika kalenda ya Kiislam). Hizi
ni Swawm kwa kumbukumbu na kumshukuru Allaah
سبحانه وتعالى kwa
kumuokoa Nabii
Muusa
a.s. pamoja na watu wake, kutokana
na Firauni na jeshi lake!
6. SWAWM NYINGINEZO
Swawm katika mwezi wa Muharram zina fadhila nyingi kama
Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alivyomweleza Abu Hurayrah.. Pia Swawm katika mwezi wa
Sha’aban, ambapo Bi ‘Aishah
رضي الله عنها
anasema kuwa Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alikuwa akikithirisha sana kufunga.
NIA
Swawm kama amali zingine, ni lazima kuwepo na Nia ndani
yake. Nia katika Swawm za Sunnah ni tofauti na Nia katika
Swawm ya mwezi wa Ramadhaan, Mwezi wa Ramadhaan Mtu
anatakiwa anuie kabla ya alfajiri. Lakini katika Swawm za
Sunnah, Nia Mtu anaweza kunuia wakati wowote, hata mchana wa
Swawm maadam hajala au hajafanya chochote kiharibishacho
Swawm toka alfajiri. Ushahidi wa jambo hili ni maelezo ya
Bi ‘Aishah
رضي الله عنها
aliposimulia kuwa Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم aliwajia
siku moja na kuwaauliza je, mna chakula chochote hapa
nyumbani? Tukasema:Hakuna!! Akawaambia kuwa: Basi Nafunga!!
Na siku nyingine alikuja akiwa amefunga (Swawm ya Sunnah),
na sisi tulikuwa tumepewa zawadi ya ‘Hais’ (aina ya chakula
alichokuwa akikipenda), nikamwambia Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
kuwa tuna ‘Hais’ tumezawadiwa hapa, nimekubakishia je,
unataka? Akasema Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
: ‘Kisogeze hapa, ingawa nilikuwa nimeamka na Nia ya kufunga
lakini nitafungua na kukila’. Kisha akasema Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم :
‘Mfano wa Swawm ya kujitolea (SUNNAH) ni sawa na Mtu ana
pesa zake, kisha akawa na khiari ya kuzitoa Sadaka au
kutozitoa”
Imepokewa na Imaam Ibn Maajah.
MUHIMU:
Ni bora watu wafahamu kuwa Nia pahala pake ni moyoni, na si
kutamka, ukishapitisha uamuzi wa kufunga, basi hiyo yatosha
na sio kukariri maneno au kutafuta mtu akufundishe namna ya
kuitamka Nia kiarabu au vinginevyo!!
WA ALLAHU A’ALAM
|