|
Amesema Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
:
((من قام رمضان إيماناً واحتساباً غفر له ما
تقدم من ذنبه))
متفق
عليه
((Atakayesimama (Kuswali) Ramadhaan kwa imaani na kutaraji
malipo, ataghufuriwa madhambi yake yaliyotangulia))
Al-Bukhariy na Muslim
Amesema Al-Haafidh ibn
Rajab, "Tambua kuwa
Muumini anajumuisha katika mwezi wa Ramadhaan jihaad mbili
kwa ajili ya nafsi yake. Jihaad ya mchana ya kufunga, na
jihaad ya usiku kwa kusimama (kuswali), atakayejumuisha
jihaad hizi mbili atapata ujira wake bila ya hesabu".
Amesema Ibn 'Uthaymiyn
"Haimpasi Muislamu
kuepukana na Swalah ya Tarawiyh katika Ramadhaan ili apate
thawabu na ujira wake, na wala asiondoke mpaka Imaam amalize
pamoja na Swalah ya Witr ili apate ujira wa Qiyaamul-Layl
yote".
Ili kuipata ladha ya
Ramadhaan na kuongeza Utiifu
na Imaan ni muhimu Muislamu ajumuike na Waislamu wenzie
kuswali Tarawiyh na kusikiliza Tilaawat ya Qur'aan
inaposomwa katika Swalah hizi kupata utulivu wa moyo na
nafsi na pia kujichumia thawabu tukufu zinazopatikana katika
kisimamo hiki na kufutiwa madhambi yake kama tulivyoona
kwenye hadiyth iliyopita.
Kwa nini
Muislamu aswali Qiyaamul-layl?
Zifuatazo ni
sababu ambazo zinampasa Muislamu azizingatie na afanye hima
kuswali Swalah ya Qiyaamul-layl ili aweze kupata fadhila
njema za kumfanya awe Muumini bora kabisa:
1)
Qiyaamul-Llayl ni Amri kutoka
kwa Allaah
سبحانه وتعالى
}}يآ
أَيُّهَا الْمُزَّمِّلُ{{
}}
قُمِ اللَّيْلَ إِلَّا قَلِيلًا{{
}}
نِصْفَهُ أَوِ انقُصْ مِنْهُ قَلِيلًا{{
}}
أَوْ زِدْ عَلَيْهِ وَرَتِّلِ الْقُرْآنَ تَرْتِيلًا
{{
{{Ewe
uliye
jifunika}}
{{Kesha usiku
kucha, ila kidogo tu!}}
{{Nusu yake,
au ipunguze kidogo}}
{{Au izidishe
- na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo}}
Al-Muzammil: 1-4
}}أَقِمِ
الصَّلاَةَ لِدُلُوكِ الشَّمْسِ إِلَى غَسَقِ اللَّيْلِ
وَقُرْآنَ الْفَجْرِ إِنَّ قُرْآنَ الْفَجْرِ كَانَ مَشْهُودًا{{
}}
وَمِنَ اللَّيْلِ فَتَهَجَّدْ بِهِ نَافِلَةً لَّكَ عَسَى أَن
يَبْعَثَكَ رَبُّكَ مَقَامًا مَّحْمُودًا{{
{{Shika Swalah
jua linapo pinduka mpaka giza la usiku, na Qur'ani ya
alfajiri. Hakika Qur'ani ya alfajiri inashuhudiwa daima}}
{{Na amka
usiku kwa ibada; ni ziada ya Sunnah khasa kwako wewe. Huenda
Mola wako Mlezi akakunyanyua cheo kinacho sifika}}
Al-Israa 78-79
Tahajjud ni Swalah inayoswalia
baada ya kulala, tunaona katika Hadiyth mbalimbali kwamba
Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alikuwa akiswali Tahajjud baada ya kulala. Nazo ni kutoka
kwa Ibn Abbaas na 'Aishah. Taz.Fathul Baari 8.83 ,
3:39
Amesema Mujaahid,
"Qiyaam kwa haki ya Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
ni Naafilah (Ziada ya Sunnah) kwa sababu ameshafutiwa
madhambi yake yaliotangulia na yaliyokuja. Na kwa haki ya
Umma wa Kiislamu Swalah ya Qiyaamul-Layl huenda ikamfutia
madhambi yake atakayotenda".
(At-Twabariy 17:525)
Na Amesema tena Allaah
سبحانه وتعالى
}}فَاصْبِرْ
عَلَى مَا يَقُولُونَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ
طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ الْغُرُوبِ{{
}}وَمِنَ
اللَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَأَدْبَارَ السُّجُودِ{{
{{Basi vumilia
kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi
kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa}}
{{Na katika
usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu}}.
Qaaf:39-40
Amesema tena:
}}وَاذْكُرِ
اسْمَ رَبِّكَ بُكْرَةً وَأَصِيلًا{{
}}
وَمِنَ اللَّيْلِ فَاسْجُدْ لَهُ وَسَبِّحْهُ لَيْلًا طَوِيلًا{{
{{Na
likumbuke jina la Mola wako
Mlezi asubuhi na jioni}}
{{Na usiku
msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu}}
Al-Insaan:25-26
2) Kumshukuru
Allaah
سبحانه وتعالى
Qiyaamul-Layl ni mojawapo ya
njia ya kumshukuru Allaah
سبحانه وتعالى
kwani kumshukuru Allaah
سبحانه وتعالى
sio
kwa kusema tu bali iwe shukurani ndani ya moyo na kukiri kwa
ulimi na kwa viungo pia kama alivyokuwa akifanya Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
وعن عائشة رضي الله عنها قالت
))
كان النبي يقوم من الليل حتى تتفطر
قدماه. فقلت له: لِمَ تصنع هذا يا رسول الله،
وقد غُفر لك ما تقدم من ذنبك
وما تأخر؟ قال: أفلا أكون عبداً شكوراً ؟
((متفق
عليه
((Imetoka kwa
Bibi 'Aishaرضي
الله عنها
kwamba
Mtume
alikuwa
akisimama
usiku hadi
ikivimba miguu yake,
nikamwambia
kwa
nini unafanya
hivi ewe Mjumbe wa Allaah, na hali umefutiwa madhambi yako
yaliyotangulia na yatakayofuatia?
Akasema,
"Nisiwe mja mwenye kushukuru?))
Al-Bukhariy
na Muslim
3) Swalah
Bora kabisa baada ya Fardh
Amesema Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
((أفضل الصلاة بعد الفريضة صلاة الليل))
رواه مسلم.
((Swalah
iliyo bora kabisa baada ya Fardh ni Swalah ya usiku))
Muslim
4) Kufufua
na kufuata Sunnah ya Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
na
Maswahaba zake
Badala ya kukesha usiku kwa
mambo mengine ya kidunia yasiyo na faida
na sisi wala Akhera yetu na kupoteza umri wetu, ni bora
kukesha kwa kumuelekea Mola Mtukufu kwa kufuata Sunnah za
kipenzi chetu Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
na
Maswahaba zake.
5)
Kubadilisha
hali ziwe kama za Salaf Swaalih
(Wema Waliopita)
Ni mwendo wa Salaf Swaalih
ambao uliendelea hadi kutufikia sisi adabu ya kutekeleza
Swalah hii ambayo ni mojawapo
wa nyenzo bora kabisa kuzidisha imani zetu, kusafisha
nyoyo zetu, kupata utulivu na kupata Ridhaa ya Allaah
سبحانه
وتعالى
6) Kujikurubisha na Allaah
سبحانه وتعالى
((وعن
عمرو بن عبسة
رضي الله عنه أنه سمع النبي
صلى الله عليه وسلم
يقول:
أقرب ما يكون الرب من العبد
في
جوف الليل الآخر فإن استطعت أن تكون ممن يذكر الله تعالى
في تلك الساعة فك))رواه
الترمذي وأبو داود.
((Imetoka kwa 'Amru bin
'Abasah
رضي الله عنهkwamba
kamsikia Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
akisema: ((Wakati Allaah Anakuwa karibu kabisa na mja, ni
wakati wa mwisho wa usiku, kwa hiyo ukiweza kuwa miongoni
mwa wanaomkumbuka Allaah
سبحانه وتعالى
katika saa hiyo basi uwe))
At-Tirmidhy na Abu Dawuud.
7) Kujikinga na uchafu wa Shaytaan
ذكر عند النبي رجل نام ليلة حتى أصبح فقال:
))ذاك
رجل بال الشيطان في أذنيه
((متفق
عليه
Alielezwa Nabii kuwa kuna mtu alilala usiku wote hadi
asubuhi bila kuswali, Akasema Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
((huyo
ni mtu aliyekojolewa na Shaytwaan katika masikio yake))
Al-Bukhariy na Muslim.
Tutaendelea
Inshaa-Allaah Ijumaa ijayo. Tumuombe Allaah
سبحانه وتعالى
Atunufaishe kwa yale
tunayojifunza na Atuajaalie ni miongoni mwa wale
wanaosikiliza kauli (nyingi) wakafuata zile zilizo njema.
Tunawaombea wote Ijumaa hii iwe ya kheri na baraka nyingi.
Aamiyn
|