TAWHIYD
    Tawhiyd

Qur'aan

Sunnah

Fiqhi

Makala

Nasiha Ya Ijumaa

Dua na Adhkaar

'Aqiyda-Tawhiyd

Vitabu

Darsa za Wanawake

    Sikiliza

Qur'aan

Mawaidha

Dua

Nashiyd

    Tizama

Video

 » Nasiha za Ijumaa  

FADHILA ZA QIYAAMUL-LAYL    (2)

Faida zake:

 1)    Wanaoswali Qiyaamul-Llayl  wameandaliwa Pepo.

Anasema Allaah سبحانه وتعالى 

}}تَتَجَافَى جُنُوبُهُمْ عَنِ الْمَضَاجِعِ يَدْعُونَ رَبَّهُمْ خَوْفًا وَطَمَعًا وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ{{

}} فَلَا تَعْلَمُ نَفْسٌ مَّا أُخْفِيَ لَهُم مِّن قُرَّةِ أَعْيُنٍ جَزَاء بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ  {{

{{Mbavu zao zinaachana na vitanda kwa kumwomba Mola wao Mlezi kwa khofu na kutumaini, na hutoa kutokana na tulivyowaruzuku}}

{{Nafsi yoyote haijui waliyo fichiwa katika hayo yanayo furahisha macho - ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda}} As-Sajdah 16-17

Aya hizi zinambashiria Pepo Muislamu mwenye kuhangaika na kujitahidi kusimama kuswali usiku  na mwenye kutoa mali yake kwa ajili ya Allaah سبحانه وتعالى, zinambashiria pepo ambayo imejaa mazuri Aliyoyaficha Allaah سبحانه وتعالى  kwa ajili yao, mazuri ya kupendeza yatakayodumu milele ambayo hajapata mtu kuyaona kwa sababu ya vitendo vyao vizuri walivyovifanya vilifichika na Allaah سبحانه وتعالى  Anaficha thawabu zao.  

ففي صحيح البخاري وغيره عن أبي هريرة رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال)): قال الله تعالى:

 أعددت لعبادي الصالحين ما لا عين رأت، ولا أذن سمعت، ولا خطر على قلب بشر، فاقرؤوا إن شئتم

 فَلاَ تَعْلَمُ نَفْسٌ مَّا أُخْفِيَ لَهُم مِّن قُرَّةِ أَعْيُنٍ جَزَاء بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ((

Al Bukhari na wengineo wamesimulia kwamba Abu Hurayrah رضي الله amesema kwamba, Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema: (("Allaah سبحانه وتعالى Amesema, Nimewatayarishia waja Wangu wema yale ambayo macho hayajapata kuona, wala masikio hayajapata kusikia, na wala hayajapata kupita katika akili ya mtu, kwa hiyo someni mkipenda   

   فَلاَ تَعْلَمُ نَفْسٌ مَّا أُخْفِيَ لَهُم مِّن قُرَّةِ أَعْيُنٍ جَزَاء بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ   

 Nafsi yoyote haijui waliyo fichiwa katika hayo yanayo furahisha macho - ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda )) As-Sajdah 16-17

Vile vile Allaah سبحانه وتعالى Ametaja Wacha Mungu watakaokuwa Peponi na yale waliyokuwa wakiyafanya, na mojawapo ni kukesha usiku kwa kufanya ibada,

}}إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ{{

}} آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَلِكَ مُحْسِنِينَ{{

}}  كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ{{

}}  وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُون{{

}}وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ{{

{{Hakika Wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na chemchem}}

{{Wanapokea aliyowapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema}}

{{Walikuwa wakilala kidogo tu usiku}}

{{Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na  asiyeomba}} Adh-Dhaariyaat: 15-19

 

2)    Sifa za Waja wa Ar-Rahmaan

}}وَعِبَادُ الرَّحْمَنِ الَّذِينَ يَمْشُونَ عَلَى الْأَرْضِ هَوْنًا وَإِذَا خَاطَبَهُمُ الْجَاهِلُونَ قَالُوا سَلَامًا  {{

}} وَالَّذِينَ يَبِيتُونَ لِرَبِّهِمْ سُجَّدًا وَقِيَامًا{{  

{{Na waja wa Ar Rahman Mwingi wa Rehema ni wale wanaotembea ulimwenguni kwa staha, na wajinga wakiwasemeza hujibu: Salama!}}

{{Na wale wanaokesha kwa ajili ya Mola  wao Mlezi kwa kusujudu na kusimama}}  Al-Furqaan: 63-64

                   

       3)      Sio sawa na wengine

}}لَيْسُواْ سَوَاء مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَآئِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللّهِ آنَاء اللَّيْلِ وَهُمْ يَسْجُدُونَ{{

{{Wote hao si sawa sawa. Miongoni mwa Watu wa Kitabu wamo watu waliosimama barabara, wanasoma Aya za Mwenyezi Mungu nyakati za usiku, na pia wanasujudu}} Al-'Imraan: 113

 }}أَمَّنْ هُوَ قَانِتٌ آنَاء اللَّيْلِ سَاجِدًا وَقَائِمًا يَحْذَرُ الْآخِرَةَ وَيَرْجُو رَحْمَةَ رَبِّهِ قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الَّذِينَ يَعْلَمُونَ

وَالَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ إِنَّمَا يَتَذَكَّرُ أُوْلُوا الْأَلْبَابِ{{

{{Je! Afanyae ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na kusimama akitahadhari na Akhera, na akitaraji rehema za Mola wake Mlezi...Sema: Eti watakuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua? Hakika wanaokumbuka ni watu wenye akili}} Az-Zumar:9               

4)    Nyakati za kughufuriwa

               Kama Anavyosema Allaah سبحانه وتعالى:  

}}الصَّابِرِينَ وَالصَّادِقِينَ وَالْقَانِتِينَ وَالْمُنفِقِينَ وَالْمُسْتَغْفِرِينَ بِالأَسْحَارِ{{

{{Wanaosubiri, wanaosema kweli, na watiifu, na wanaotoa sadaka, na wanaoomba maghfira kabla ya alfajiri}} Al-'Imraan 17

        Vile vile:

 ((عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ينزل ربنا تبارك وتعالى كل ليلة إلى السماء

الدنيا حين يبقى ثلث الليل الآخر  فيقول: من يدعوني فأستجيب له؟ من يسألني فأعطيه؟ من يستغفرني فأغفر له))

 رواه الجماعة.

((Imetoka kwa Abu Hurayra رضي الله عنه kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم  ِAmesema: Allaah سبحانه وتعالى Huteremka kila siku katika mbingu ya dunia (mbingu ya kwanza) inapobakia thuluthi ya mwisho ya usiku na Husema: Nani ananiomba Nimtakabalie? Nani Ana shida nimtekelezee? Nani ananiomba maghfira Nimghufurie?)) Imesimuliwa na Jama'a  

5)      Siha kwa mwili

 ((عليكم بقيام الليل فإنه دأب الصالحين قبلكم، وقربة إلى الله تعالى، ومكفرة للسيئات، ومنهاة عن الإثم،

ومطردة للداء عن الجسد )) رواه أحمد والترمذي وصححه الألباني

((Shikamaneni na kusimama (kuswali) usiku kwani ni tabia/adabu za waja wema kabla yenu, na kujikurubisha kwa Allaah سبحانه وتعالى , na ni kafara ya maovu, na ni kinga ya dhambi, na ni kiondosho cha maradhi katika mwili)) Ahmad na At-Tirmidhiy na kaisahihisha Albaniy

6)     Nyakati ya kukubaliwa dua'a

                 Amesema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم :

 ((ان في الليل لساعة لا يوافقها رجل مسلم يسأل الله  تعالي خيرا من امر الدنيا  و الاخرة، الا اعطاه اياه،

 وذلك كل ليلة))  رواه مسلم

((Hakika katika usiku kuna saa ambayo mja anapomuomba Allaah سبحانه وتعالى  kheri katika mambo ya dunia au Akhera ila (Allaah) Humpa kheri hizo, na hivyo ni kila usiku)) Muslim

7)    Usharifu (Utukufu) wa Mu'mim

               Kama alivyosema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم:

((أتاني جبريل فقال: يا محمد، عش ما شئت فإنك ميت، وأحبب من شئت فإنك  مفارقه، واعمل ما شئت فإنك

مجزي به، واعلم أن شرف المؤمن قيامه بالليل، وعزه استغناؤه عن الناس  ))

 رواه الحاكم والبيهقي وحسنه المنذري والألباني

((Amenijia Jibriyl akasema: Ewe Muhammad ishi upendavyo bila shaka wewe ni maiti (utakufa), na mpende umtakaye bila shaka utafarikiana naye, na tenda unavyopenda lakini ujue utalipwa kwa vitendo hivyo, na tambua kwamba utukufu wa Muumin ni Qiyaamul-Llayl, na heshima yake ni kujitosheleza Na watu))

Al Haakim na Al Bayhaqiy, na Al Mundhiriy na Albaaniy wamesema ni Hadiyth Hasan

 

8)    Husnul-Khaatimah (Mwisho Mwema)  

 ((من قام بعشر آيات لم يُكتب من الغافلين، ومن قام بمائة آية كتب من القانتين، ومن قام بألف آية كتب من المقنطرين ((

رواه أبو داود وصححه الألباني (والمقنطرون هم الذين لهم قنطار من الأجر)

((Atakayesimama (usiku) na aya kumi hatoandikiwa katika miongoni mwa walioghafilika, na atakayesimama kwa aya mia ataandikiwa ni miongoni mwa wanyenyekevu, na atakayesimama kwa aya Alfu ataandikwa miongoni mwa wenye mirundi)) Abu Dawuud na amesahihisha Albaniy (Maana ya mirundi ni wale walio na mrundi wa thawabu)

 

9)      Uso hung'ara  kwa Nuru

يقول الحسن البصري رحمه الله : " لم أجد من العبادة شيئا أشد من الصلاة  في جوف الليل"  فقيل له :

 ما بال المجتهدين من أحسن الناس وجوها فقال: "لأنهم خلوا بالرحمن فألبسهم من نوره" 

Anasema Hasan Al Baswry Mwenyeezi Mungu Amrehemu: "Sijapata kuona ibada iliyo nzito kama Swalah katika kiza cha usiku". Akaulizwa, Vipi wale watu wajitahidio wenye nyuso nzuri kabisa? Akajibu, "kwa sababu wamejitenga (wamejifaraghisha na) Na Ar-Rahmaan, basi Naye Akawavisha Nuru Yake" .

Sababu za kukuwezesha kuamka Qiyaamul-layl

a)  Usile na kunywa hadi ukashiba sana usiku.

b)  Usijitaabishe sana mchana kwa yasiyo na faida.

c)  Usiache 'Qaylulah' (kulala kidogo mchana) kwani inasaidia   kuamka usiku.

d) Usifanye maasi kwani yanamzuia mtu kuamka Qiyaamul- layl.

e) Safisha moyo wako kutokana na uhasidi, chuki na waislamu wenzako.

f)  Fikiria mauti na usiwe na matumaini ya kuishi sana.

g) Tambua fadhila zake.

 

Tutaendelea Inshaa-Allaah  Ijumaa ijayo. Tumuombe Allaah سبحانه وتعالى   Atunufaishe kwa yale tunayojifunza na Atuajaalie ni miongoni mwa wale wanaosikiliza kauli (nyingi) wakafuata zile zilizo njema.

Tunawaombea wote Ijumaa hii iwe ya kheri na baraka nyingi. Aamiyn