Muislam anapofanya maasi ni lazima atubie haraka
iwezekanavyo kuonyesha kuwa ametambua makosa
yake, na hapo ndipo atakapokuwa amedhamiria kwa
nia
}}إِنَّمَا
التَّوْبَةُ عَلَى اللّهِ لِلَّذِينَ يَعْمَلُونَ
السُّوَءَ بِجَهَالَةٍ
ثُمَّ يَتُوبُونَ مِن قَرِيبٍ فَأُوْلَـئِكَ
يَتُوبُ اللّهُ عَلَيْهِمْ
وَكَانَ اللّهُ عَلِيماً حَكِيماً{{
{{Hakika
toba inayo kubaliwa na Mwenyezi Mungu ni ya wale
wafanyao uovu kwa ujinga, kisha wakatubia kwa
haraka. Hao ndio Mwenyezi Mungu huwakubalia toba
An-Nisaa 17
Kuchelewa kuomba Tawbah
huenda
kusifae tena
Huenda mtu akaendelea kufanya madhambi hadi
akafika wakati wa kukata tamaa ya kuishi na
wakati wa kuiaga dunia umekaribia ndipo
akatambua umuhimu wa kuomba tawbah kwa Mola
wake, hapo tena atakuwa kachelewa kabisa na hapo
tawbah yake itakuwa haina faida tena
}}وَلَيْسَتِ
التَّوْبَةُ لِلَّذِينَ يَعْمَلُونَ السَّيِّئَاتِ
حَتَّى إِذَا حَضَرَ
أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ إِنِّي تُبْتُ الآنَ
وَلاَ الَّذِينَ
يَمُوتُونَ وَهُمْ كُفَّارٌ أُوْلَـئِكَ
أَعْتَدْنَا لَهُمْ عَذَابًا
أَلِيمًا{{
{{Wala
hawana toba wale wafanyao maovu mpaka yakamfikia
mmoja wao mauti, kisha hapo akasema: Hakika mimi
sasa nimetubia. Wala wale wanao kufa na hali wao
ni makafiri. Hao tumewaandalia adhabu chungu }}
An-Nisaa 18
Mfano mzuri tunao
katika Qur'aan wa Fir'awn kama alivyofanya
wakati anazama na hapo ndio akaona hana hila
tena ndio akaomba tawbah,
}}وَجَاوَزْنَا
بِبَنِي إِسْرَائِيلَ الْبَحْرَ فَأَتْبَعَهُمْ
فِرْعَوْنُ وَجُنُودُهُ
بَغْيًا وَعَدْوًا حَتَّى إِذَا أَدْرَكَهُ
الْغَرَقُ قَالَ آمَنتُ
أَنَّهُ لا إِلِـهَ إِلاَّ الَّذِي آمَنَتْ بِهِ
بَنُو إِسْرَائِيلَ
وَأَنَاْ مِنَ الْمُسْلِمِينَ{{
{{Tukawavusha
bahari Wana wa Israili, na Firauni na askari
wake wakawafuatia kwa dhulma na uadui. Hata
Firauni alipo kuwa anataka kuzama akasema:
Naamini kuwa hapana mungu ila yule waliye
muamini Wana wa Israili, na mimi ni miongoni mwa
walio nyenyekea!}}
Yunus
90
Allaah
سبحانه وتعالى
Akamuuliza Fir'awn wakati anatapatapa na kuomba
na kudai kuwa kaamini:
}}آلآنَ
وَقَدْ عَصَيْتَ قَبْلُ وَكُنتَ مِنَ
الْمُفْسِدِينَ{{
{{Alaa! Sasa? Na hali uliasi kabla yake na ukawa
miongoni mwa mafisadi!}}
Yunus 91
Kisha Akaikataa
Tawbah yake katika hali hii:
}}فَالْيَوْمَ
نُنَجِّيكَ بِبَدَنِكَ لِتَكُونَ لِمَنْ خَلْفَكَ
آيَةً وَإِنَّ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ عَنْ
آيَاتِنَا لَغَافِلُونَ{{
{{Leo,
basi, tutakuokoa kwa mwili wako, ili uwe Ishara
kwa ajili ya walio nyuma yako. Na hakika watu
wengi wameghafilika na Ishara zetu}}
Yunus
92
Mtume
صلى الله عليه وسلم
vile vile hakuaacha kutufahamisha hatari ya
kuchelewa kuomba tawbah kama katika hadithi
zifuatazo zinavyoonyesha:
Kuomba
tawba kabla ya sakaraatil-maut
((قال صلى الله عليه وسلم: إن الله يقبل توبة
العبد ما لم يغرغر))
رواه أحمد والترمذي وصححه النووي
))Hakika
Allaah
سبحانه وتعالى
huikubali toba ya mja wake kabla ya roho kufika
kwenye mkoromo wa mauti))
Imesimuliwa na Ahmad na Kusahishwa na An-Nawawy
Na Kabla ya kuchomoza jua upande wa Magharibi
((عن أبي هريرة رضي الله عنه أن النبي صل قال :
من تاب قبل أن تطلع الشمس من مغربها تاب الله
عليه))
رواه مسلم
((Kutoka kwa Abu Hurayra
رضي الله عنه
kwamba Mtume
صلى الله عليه وسلم
kasema, "Atakayetubu
kabla ya kuchomoza jua upande wa Magharibi,
Allaah
سبحانه وتعالى
Atamkubalia toba yake"))
Muslim
Kabla ya moyo kupofuka wote
Hatari nyingine ni kuwa huenda ikampofoa mtu
moyo wake akawa hajali tena kufanya maovu na
hata ikawa shida tena mtu huyo kupata uongofu ,
huwa haoni hasikii yumo katika maasi. Hadithi
ya Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
inasema kuhusu hili:
((عن أبي هريرة رضي الله عنه ، قال: قال رسول الله
صلى الله عليه وسلم: إن العبد إذا أذنب ذنباً نكت
في قلبه
نكتة سوداء ، فإذا تاب ونزع واستغفر صُقل قلبه ،
وإن زاد زادت حتى تعلوا قلبه
، فذلك الران الذي ذكره الله عز وجل
}}كَلاَّ
بَلْ رَانَ عَلَى قُلُوبِهِم
مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ
({{ (
المطففين :) رواه أحمد والترمذي وحسنه
الألباني
((Imetoka
kwa Abu Hurayra
رضي الله عنه
Mja anapofanya dhambi, doa jeusi (kutu) huwekwa
katika moyo wake. Akiacha dhambi hiyo, na
kuomba maghfira na kutubu, moyo wake husafishwa
ukawa msafi, lakini akirudia kufanya dhambi, doa
(kutu) huzidi kuenea mpaka kufunika moyo wote
na hiyo ndio 'Raan' (kutu) aliyosema Allaah
سبحانه وتعالى
{{
Sivyo hivyo! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao
(maovu) waliyokuwa wakiyachuma}}
(Al-Mutaffifiin
14)
))
Imesimuliwa na Ahmad, At-Tirmidhi na Sheikh Albaani kasema ni hadithi Hassan

