TAWHIYD
    Tawhiyd

Qur'aan

Sunnah

Fiqhi

Makala

Nasiha Ya Ijumaa

Dua na Adhkaar

'Aqiyda-Tawhiyd

Vitabu

Darsa za Wanawake

    Sikiliza

Qur'aan

Mawaidha

Dua

Nashiyd

    Tizama

Video

 »  Nasaha  

IJAALIE NYUMBA KUWA NI SEHEMU YA KUMTAJA ALLAH(SW)

 Anasema Mtume (SAW) katika hadithi kwamba:

 

مثل البيت الذي يذكر الله فيه ، والبيت الذي لا يذكر الله فيه مثل الحي والميت.

Mfano wa nyumba ambayo anatajwa Allah(SW) (kwa kukumbukuwa)  ndani yake na mfano wa nyumba asiotajwa Allah(SW) ni sawa na mtu alie hai na maiti

 

Hatuna budi ndugu zangu waislamu kukumbushana  na kunasihiana kwamba nyumba zetu zijengwe kwa misingi ya kuwa ni sehemu za ibada pia licha ya kuwa sehemu za kujipumzisha na kujisitiri.

 

Tunatakiwa tuutumie vizuri wakati tupo majumbani pamoja na familia zetu kwa

 

1.   Kumtaja Allah(SW) ,

2.   Kumkumbuka ikiwa ndani ya nyoyo zetu au kwenye ndimi zetu.

3.   Kusali sala za sunna(za fardhi lazima zisaliwe misikitini) .

4.   Kusoma/kusikiliza/kujifunza/kufundisha Quraan

5.   Kujifunza mambo mengi ya dini yetu kwa kusoma vitabu vya kidini .

6.   Kujenga mazoea ya  kutazama/kusikiliza kanda za mawaidha na dvd za kiislamu

 

Vyenginevyo nyumba zetu ikiwa hazitajwi wala kukumbukwa Allah(SW) zitakuwa kama alivyozielezea Mtume(SAW) “maiti”. Hazina uhai kwa kukosekana utajo wa Allah(SW) ndani  yake na moja kwa moja kuingiliwa na shetani alielaaniwa na kukimbiwa na malaika. Hivyo kupatikana ndani yake kila aina ya uchafu na balaa ambalo kwa jinsi shetani anavyoyazaini na kuyapamba huonekana kuwa ni mambo mazuri.

 

Hivyo ni wajibu kuzihuisha nyumba zetu na kumtaja na kumkumbuka Allah(SW) kila tupatapo wasaa wa kufanya hivyo.

 

Wabillahi Tawfiq