Maana ya tawbah ni kurudi. Na tawbah inaanza mtu
anapoanza kukumbuka madhambi yake, akaingiwa na
khofu ya kughadhibikiwa na Mola wake, kisha
khofu yake ikampelekea kurudi kwa Allaah
سبحانه وتعالى
na kumuomba Amsamehe makosa yake.
Na tawbah vile vile ni ibada, haghafiliki nayo
mja mwema, hata Mitume ya mwanzo walikuwa
wakiomba tawbah. Kwa hiyo sio khasa kwa
wafanyao dhambi tu bali hata kwa waumini, kwani
wao pia kuomba tawbah ni sababu ya kufaulu kwao
ndio maana Allaah
سبحانه وتعالى
kasema:
}}
وَتُوبُوا إِلَى اللَّهِ جَمِيعًا أَيُّهَا
الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ{{
{{Na tubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi
Waumini, ili mpate kufanikiwa}}
An-Nuur 31
Baadhi ya watu wanafikiri kuwa tawbah ni kwa
sababu ya madhambi makubwa pekee, wakati hakika
kila mtu anahitaji kuomba tawbah usiku na mchana
kwani madhambi mangapi madogo madogo mtu
anayafanya mengine bila ya kujijua atakuja
kuyakuta katika daftari
Muislam
anapofanya maasi ni muhimu kurudi kwa Mola Wake
aombe maghfira na tawbah ili airudishe nafsi
yake katika kutoharika. Na Allaah
سبحانه وتعالى
yuko tayari kabisa kupokea tawbah zetu na
kutusamehe maovu yetu.
}} وَهُوَ
الَّذِي يَقْبَلُ التَّوْبَةَ عَنْ عِبَادِهِ
وَيَعْفُو عَنِ السَّيِّئَاتِ{{
{{Naye ndiye anaye pokea toba kwa waja wake, na anasamehe makosa}} As-Shura 25
Je, nani aliyejidhulumu nafsi yake akawa hana
raha na makosa aliyoyafanya? Je, hajui mtu kuwa
Allaah
ni Mwingi wa Kusamehe na Mwingi wa Rahma?
}}وَمَن
يَعْمَلْ سُوءًا أَوْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ ثُمَّ
يَسْتَغْفِرِ اللّهَ يَجِدِ اللّهَ غَفُورًا
رَّحِيمًا{{
{{Na
anaye tenda uovu au akajidhulumu nafsi yake,
kisha akaomba maghfira kwa Mwenyezi Mungu,
atamkuta Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghfira,
Mwenye kurehemu}}
An-Nisaa 110
Na
}}وَاسْتَغْفِرُواْ
رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُواْ إِلَيْهِ إِنَّ رَبِّي
رَحِيمٌ وَدُودٌ{{
{{Na
ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi, tena tubuni
kwake. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye
kurehemu na Mwenye upendo}}Huud
90
Na kwa Rahma yake Allaah
سبحانه وتعالى
hakutuamrisha tu tuombe tawbah bali na
kutuamrisha pia kukimbilia kuomba hiyo tawbah
Kwake
}}وَسَارِعُواْ
إِلَى مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ{{
{Na
yakimbilieni maghfira ya Mola wenu Mlezi}}
Al-'Imraan 133
Lakini mtu anapofanya maasi ni lazima atubie haraka bila ya kusubiri kwani kuna hatari kubwa ya kuchelewa kuomba tawbah.

