">
TAWHIYD
    Tawhiyd

Qur'aan

Sunnah

Fiqhi

Makala

Nasiha Ya Ijumaa

Dua na Adhkaar

'Aqiyda-Tawhiyd

Vitabu

Darsa za Wanawake

    Sikiliza

Qur'aan

Mawaidha

Dua

Nashiyd

    Tizama

Video

 » Mengineyo  

Mahitajio Ya Nafsi

Mahitajio ya miili yetu  (chakula) yote  hutoka ardhini ambako ndio asili ya kuumbwa huu mwili.

 

الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الأََرْضَ مَهْدًا وَسَلَكَ لَكُمْ فِيهَا سُبُلاً وَأَنزَلَ مِنَ السَّمَاء مَاء فَأَخْرَجْنَا بِهِ أَزْوَاجًا مِّن نَّبَاتٍ شَتَّى ﴿53﴾ كُلُوا وَارْعَوْا أَنْعَامَكُمْ إِنَّ فِي ذَلِكَ لأَيَاتٍ لأُُوْلِي النُّهَى ﴿54﴾ مِنْهَا خَلَقْنَاكُمْ وَفِيهَا نُعِيدُكُمْ وَمِنْهَا نُخْرِجُكُمْ تَارَةً أُخْرَى ﴿55﴾

{{Ambaye amekufanyieni ardhi kuwa tandiko, na akakupitishieni humo njia, na akakuteremshieni kutoka mbinguni maji. Na kwa hayo tukatoa namna mbali mbali za mimema}}.

 

{{Kuleni, na mchunge wanyama wenu. Hakika katika hayo zipo ishara kwa wenye akili}}.

 

{{Kutokana nayo (ardhi) tumekuumbeni, na humo tunakurudisheni, na kutoka humo tutakutoeni mara nyengine}}.

Taha: 53 - 55

Nafsi hali kadhalika mahitajio yake nayo yanotakana na asili yake ambayo ni kutoka juu kwa Allaah سبحانه وتعالى .  Kwa hiyo, vitu viwili hivi visipopata mahitajio yake utaona kuwa vinadhoofika.   Mwili huenda mtu akakonda na kuumwa kwa kutokupata chakula cha siha, na nafsi ikikosa mahitaji yake ambayo ni kuwasiliana na kuambatana na Allaah سبحانه وتعالى kwa kila aina ya ibada na dhikr, basi nayo hudhoofika ndio utamuona mtu yuko kwenye maovu tu, nafsi yake iko mbali na Mola wake, nafsi nyingine hata haijamtambua Mola wake. Na kwa mwenye kumjua vile vile kama sisi Waislamu tunaomuamini Allaah سبحانه وتعالى, ikiwa hatuipi nafsi zetu mahitajio yake ndio utamuoma mtu vile vile yuko kwenye maasi na mwengine japo hafanyi maasi lakini yuko kwenye dhiki fulani, hana raha kwa vile ameikosesha nafsi yake mahitajio yake.

Ibada na vitendo vyenye kuambatana na Allaah سبحانه وتعالى

Jambo la kwanza la  kuambatana na Allaah سبحانه وتعالى ni kuitoharisha nafsi  kwa  kuomba maghfira na kutubu.

Maghfira na toba (tawbah)


 

Kwa vile binaadamu sote ni wenye kufanya makosa kila siku kama alivyosema Mtume صلى الله عليه وسلم

((كل بني آدم خطاء، و خير الخطائين التوابون)) حسن الألباني صحيح الجامع

((Kila Binaadamu ni mkosa na mkosa mbora kabisa ni yule anayeomba toba)).  Ameseme Sh Albani ni Hadithi Hassan kutoka Sahihil-Jaami'i  

Kwa Rahma ya Allaah سبحانه وتعالى hata binaadamu awe ana makosa vipi, huenda akafutiwa dhambi zake zote, kwa hiyo mtu asikate tamaa au kukhofu kuwa dhambi zake hazitofutwa. 

 

 

قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَى أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّهِ إِنَّ اللَّهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ ﴿53﴾

{{Sema: Enyi waja wangu walio jidhulumu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu}} Az-Zumar: 53

 

Allaah سبحانه وتعالى Ametuamrisha tumuombe toba katika aya nyingi za Qur'aan kama mfano wa aya hizi zifuatazo:  

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا تُوبُوا إِلَى اللَّهِ تَوْبَةً نَّصُوحًا ع

{{Enyi mlio amini! Tubuni kwa Mwenyezi Mungu toba iliyo ya kweli!}}  At-Tahriim 8

وَتُوبُوا إِلَى اللَّهِ جَمِيعًا أَيُّهَا الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ

 

{{Na tubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate  kufanikiwa}} 

 An-Nuur : 31