|
Suala
la malezi ni suala muhimu. Ni suala ambalo kila mmoja wetu amekutana nalo na
bado yupo katika kuendelea nalo.Kwa atakaefanikiwa ni yule atakaelea
watoto wake malezi sahihi ya kiislamu INSHAALLAH.
Mlezi
anaweza kuwa mzazi halisi (baba na mama) anaweza kuwa mwalimu chuoni au skuli na
pia yoyote yule ambao amejikuta katika hali ya kulea ikiwa kama ni mtoto wake au
wa mtu mwengine. Ikiwa kila mmoja kati ya hawa atatekeleza jukumu lake vilivyo
katika kulea, kuelimisha , kuongoza na kurekebisha ; jamii ya kiislamu nayo
ingeliongoka na kuwa ya kupigiwa mfano katika tabia na “akhlaaq” maadili.
Na kama
moja kati ya viungo hivi muhimu vya malezi vitazembea katika majukumu yake hapo
pia kuna hatari kwa jamii ya kiislamu kupotoka kwa kukosa msingi mzuri wa malezi
sahihi ya kiislamu .
Viungo
vyote hivyi vinategemeana . Mzazi/mlezi humtegemea Mwalimu kwani jukumu
analolitekeleza Mwalimu na kwa niaba ya mzazi. Na Mwalimu humtegemea mzazi/mlezi
kwa kuhakikisha mafundisho anayoyapata mtoto; mzaz/mlezi ana wajibu wa
kuhakikisha yanafanyiwa kazi .
Lengo
kuu la malezi ni katika uislamu ni kumjenga anaelelewa kuwa mfano wa hali ya juu
katika jamii. Anatakiwa aandaliwe kujifunga na mola wake, kuwa karibu na mola
wake kwa kila jambo analolifanya . Kuandaliwa kuwa na tabia nzuri ambazo
kila muislamu hutakiwa kujipamba nazo kama vile alivyojipamba nazo Mtume wetu
(SAW).Kuandaliwa kuweza kuishi katika jamii, kujenga mahusiano mazuri kati yake
na wazazi, ndugu na jamaa, rafiki, walimu, majirani na watu wote kwa ujumla .
Kuandaliwa vyema mpaka ukifika wakati wa kukabidhiwa majukumu(mukallaf) anakuwa
tayari kuyabeba na kuyatekeleza kikamilifu kwa mujibu wa sheria n.k. Na pia
kuandaliwa na kuweza kujua nafasi yake katika maisha mafupi yatakayomkabili na
lengo la kuletwa katika ulimwengu huu. Kwa ufupi maandalizi haya yanakuwa katika
kiwiliwili, kiakili, kitabia na kiroho.
Inshaallahu Taala katika page yetu hii ya malezi tutajaribu kumuomba Allah atupe
uwezo wa kujaribu kuwafundisha walezi wetu maadili mema katika malezi, utaratibu
mzuri katika kulea na kutoa “directives” miongozo katika mfumo mzuri wa malezi
hasa kwa ndugu zetu wanaoishi nchi hizi za kimagharibi ambao wengi wao kwa
bahati mbaya wanapata taabu katika suala zima la malezi kwa sababu ya kuwepo
katika nchi ambazo mfumo wao wa malezi upo tofauti kabisa na mfumo wetu. Pia kwa
kukosa watu wa kuwaongoza kukabiliana na mtihani huu mzito kwani mara nyingi
hujaribu kutafuta ushauri nyumbani(Africa) lakini kwa sababu tayari mazingira ni
tofauti ushauri huu unakuwa mara nyingi ni vigumu kutekelezeka.
Wabillahi Tawfiq
|