|
YANAYOBATILISHA (YANAYOHARIBU) SWAWM
1. Kula na kunywa kwa makusudi. Na sio kwa kusahau wala kwa
bahati mbaya au kwa kulazimishwa, katika mchana wa Swawm.
2. Kujitapisha kwa makusudi. Kuwe kujitapisha huko kwa kutia
kidole mdomoni au kunusa kitu kitachopelekea kutapika.
3. Mume kumuingilia Mke wake. Na pia kumkumbatia au kumchezea
hadi yakamtoka manii.
4. Kujichua (kuyatoa manii) kwa makusudi ima kwa mkono au kwa
kuchezewa na Mkeo au kwa njia yoyote ile. Ama manii hayo
yakitoka kwa kuota (ndoto) au kutazama (bila kukusudia)
basi haiharibu Swaumu.
5. Kupatwa na Hedhi au Nifasi kwa Mwanamke. Hata kukiwa
kutokea huko kuwa ni wakati wa kukaribia kufuturu.
6. Mwenye kutia Nia ya kula wakati amefunga, kwa sharti kuwa
kaazimia tendo
hilo hata kama hakulitekeleza.
7. Kudhania kuwa jua lishazama magharibi au bado
hakujapambazuka (yaani haujaanza wakati wa kufunga),
kisha akala ,akanywa au akamuingilia mke wake.
YASIYOBATILISHA
(YASIYOHARIBU) SWAWM
1. Kula au kunywa kwa kusahau, kimakosa au kulazimishwa.
2 Kuingia maji ndani ya matundu ya mwili bila kukusudia, kwa
mfano wakati wa kuoga.
3
Kudungwa sindano mwilini wakati wa maradhi.
4
Dawa ya maji idondoshewayo machoni.
5
Kuoga na kujimwagia maji mwilini wakati wa joto kali.
6 Kuonja chakula kwa mpishi kwa sharti asimeze kile
akionjacho.
7 Kumbusu au kumkumbatia mkeo, kwa sharti awe mtu ana uwezo
wa kujizuia na kudhibiti matamanio yake.
8 Kupiga chuku (cupping), ikiwa kupika chuku huko
hakutomfanya huyo mtu adhoofike. Ingawa kuna baadhi ya
Maulamaa wanaona kuwa haifai.
9 Haitobatilika swawm ya mtu atakayeamka na janaba au
atakayeota mchana wa swawm akatokwa na manii.
10 Kuingia harufu ya manukato au udi puani mwake. Ingawa baadhi
ya Maulamaa wanasema ni vizuri kujiepusha moshi usiingie
hadi kufika tumboni.
11 Kupiga mswaki, kusukutua au kusafisha pua kwa kutia maji
puani bila kuzidisha.
DUA
YA KUFUTURU
عن عبد الله بن عمر رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه
وسلم كان إذا أفطر قال: () ذهب الظمأ وابتلت العروق، وثبت الأجر
إن شاء الله
)) رواه أبو داود والنسائي بإسناد حسن .
Kutoka kwa Abdullah bin ‘Umar
رضي الله عنه ambaye amesema, Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alipokuwa akifungua, anasema: ((Kiu kimeondoka, na
mishipa imelainika, na yamethibiti malipo Mwenyeezi
Mungu Akipenda)). Imesimuliwa na Maimam Abu Dawuud na An
Nasaaiy.
KUFUNGUA
KWA TENDE AU MAJI
قال رسول الله صلى الله عليه وسلم ((من وجد التمر فليفطر
عليه ، ومن لم يجد التمر فليفطر على
الماء ، فإن الماء طهور))
رواه أحمد وأبو داود والترمذي
Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
amesema:((Atakayepata tende afuturu kwayo, na asiyepata
basi afungue kwa maji, kwani maji ni tohara)) Imesimuliwa na Maimamu Ahmad, Abu Dawuud na At Tirmidhy
FADHILA YA DUA WAKATI WA KUFUNGUA
قال رسول الله صلى الله عليه وآله وسلم ((للصائم عند فطره
دعوة لا ترد ))
رواه ابن ماجة
Amesema Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
((Mwenye kufunga dua yake hairudishwi wakati wa kufuturu)).
Imesimuliwa na Imam Ibn Maajah
WATU
WALIORUHUSIWA KUTOFUNGA
Kufunga Ramadhaan ni Fardh kwa kila
Muislam
aliye baaligh, mwenye akili
timamu
isipokuwa kwa wale kufunga ni shida na itawaletea
madhara nao ni wenye udhuru kama huu ufuatao:
1) Walio katika safari na wagonjwa ambao kufunga kwao
kutawafanya wawe wagonjwa zaidi, haipendezwi
kwa watu hao kufunga, lakini wakifunga Swawm yao
itakubaliwa. Wakichagua au kupenda kuwa wasifunge basi
ni lazima walipe siku hizo wasizofunga baada ya
Ramadhaan.
2) Wanawake walio katika hedhi na waliotoka kuzaa
ambao wako katika damu ya Nifaas
hawaruhusiwi kufunga, na wakifunga katika hali hii, basi
Swawm yao haitokubaliwa. Nao pia ni lazima walipe kila
siku walizoacha baada ya Ramadhaan.
3) Wanawake wajawazito na wanaonyonyesha ikiwa watakhofu kuwa
Swawm itawadhuru watoto wao au wenyewe, hao sio lazima
kufunga. Lakini ikiwa hawatafunga Ramadhaan basi ni
lazima wafunge baada ya Ramadhaan kulipa siku zao.
Na ikiwa waliacha kufunga kwa sababu tu ya kukhofia afya
ya watoto wao, basi wanapaswa kulipa na kumlisha maskini
mmoja kwa kila siku moja iliyowapita katika Ramadhaan.
4) Watu wasioweza kufunga kutokana na umri mkubwa
na maradhi yasiyopona hawatakiwi kufunga. Inawatosheleza kulisha
maskini mmoja kwa kila siku moja wanayoshindwa kufunga.
Na kila wakiweza kulisha maskini zaidi ni bora.
TUNAWAOMBEA KILA LA KHERI KATIKA MWEZI MTUKUFU
WA RAMADHAAN. MWENYEEZI MUNGU AUJAALIE UWE WA KHERI NA
MAVUNO INSHAALLAH
|