TAWHIYD
    Tawhiyd

Qur'aan

Sunnah

Fiqhi

Makala

Nasiha Ya Ijumaa

Dua na Adhkaar

'Aqiyda-Tawhiyd

Vitabu

Darsa za Wanawake

    Sikiliza

Qur'aan

Mawaidha

Dua

Nashiyd

    Tizama

Video

 » Sunnah  

MJADALA WA MWANDAMO WA MWEZI

Vijana wa Salafiyya - Dar-es-salaam

Namshukuru Allah (sw), sala na amani juu ya Mtume wetu  Muhammad (s.a.w.) huu ni mtazamo  kwa ufupi jinsi ya kuingiya kwa mwezi wa Ramadhani na kufunga na kutoka kwa mwezi wa Ramadhani na kufunguliya.

 

Ndugu Muisilamu mas-ala ya mwandamo wa mwezi yameleta mijadala na mipasuko mikubwa miyongoni mwetu Waislamu kila mmoja anajaribu kuleta hoja zake kuhalalisha mitazamo yake namna ya kufunga wengine wanasema kufunga ni mwezi ukionekana popote pale ulimwenguni wengine wanasema kila nchi ina machimbuko yake ya mwezi.  InshaAllah katika makala hayo uliyo nayo  mbele yako hivi sasa tutajaribu kukaguwa hoja za pande zote mbili ili ninyi wenyewe Waislamu mjionee haki iko wapi bila kujiingiza katika ushabiki usiyo na maana yoyote. Tafadhali soma kwa makini hoja zote ili uchukuwe maamuzi mwenyewe.

 

Wapendwa Waislamu  mas-ala ya kufunga na kufunguwa yametundikwa kwa kuonekana mwezi haturuhusiwi waislamu kufunga na kufunguwa mpaka uonekane mwezi au tukamilishe siku 30. Na huu mwezi una kazi kubwa sana  na manufaa mengi  katika maisha ya mwanadamu miyongoni mwa manufaa ni hili suwala la kutekeleza Ibada na funga ya mwezi wa Ramadhani na kuna manufaa mengine mengi lakini hatuwezi kuelezeya manufaa yote  hayo kwa kuwa  siyo dhumuni letu.

 

Kwanza kabisa kuhusu suwala la mwezisayari ndugu Muislam mwezisayari umetajwa ndani ya Qu-r an zaidi ya mara 25 lakini leo sisi tutachukuwa  aya sita tu ambazo zinazungumziya huu mwezisayari. Ya kwanza kasema  Mwenyezi Mungu:

 

 (Ndiye anayepambazuwa asubuhi na umeufanya usiku kuwa mapumziko na juwa na mwezi kwenda kwa hesabu…)Qur-an 6:96.

 

Ushahidi juu ya aya hii kuwa mwezisayari umeumbwa kwa ajili ya mahesabu. Kasema tena:

 

 (Yeye Mwenyezi.Mungu Ndiye aliyelifanya juwa kuwa mwanga na mwezi kuwa nuru na akaupimia vituwo (huwo mwezi)ili mjue Idadi ya miyaka na hesabu (nyinginezo)…)Qur-an 10:5

 

Hapa tunapata wazi kuwa mwezisayari una vituo na madhumuni ya kuumbwa kwake  tupate kujuwa idadi ya miyaka kwa kupitia hesabu za kila mwezi  siku kwa kuonekana kwa huo mwezisayari. Kasema tena M.Mungu:

 

(Na mwezi kadhalika ni alama kwao tumeupimiya vituwo (hiki baada ya hiki) mpaka unakuwa (mwembamba) kama chaparare la mtende kuukuu (lililonywea) Qur-an 36:39.

 

 

Hapa vile vile M.Mungu anatuelezeya kuwa  mwezisayari una vituo na hivyo vituwo ndiyo Idadi ya hesabu ya masiku yetu. Na kasema tena:

 

(Na juwa na mwezi (huenda) kwa hesabu (yake)).Qur-an 55:5

 

Hapa vile vile tunapata kuwa huu mwezisayari hutembea katika vituo vyake alivyovipangilia Mwenyezi Mungu. kasema tena:

 

 (Na kwa mwezi unapokamilika) Qur-ani84:18

 

Hapa Mwenyezi Mungu anaapa kwa mwezisayari unapokamilika , kwa hiyo hapa kuna dalili ya wazi kuwa mwezisayari unakuwa mdogo mpaka unakamilika na halafu unarudi kuwa mdogo kasema  tena MwenyeziMungu:

 

 (Na kwa mwezi unapoliandama) Qur-an 91:2.

 

 Hapa vilevile M.Mungu anaapa kwa mwezisayari  unapoandama unapokamilisha mahesabu ya vituwo vyake na kuanza upya. Ndugu Muislaam sasa tuvitazame vituwo vya mwezisayari je  kuna vituo vingapi?

          

Majina ya vituwo 10 vya mwezisayari

 

Ndugu Muislam mwezisayari una vituwo 10 katika mwezi mzima kama alivyosema MwenyeziMungu

 

 (…Na mwezi kuwa nuru na akaupimiya vituwo….)

 

na vituwo vyote kwa lugha ya kiarabu kila kituwo kina jina lake, tukianza kituo 1-3 kinaitwa Ghurar, kituwo 4-6 kinaitwa Nuqal, kituwo cha 7-9, kinaitwa Tus’o, na kituwo 10-12 U’shru, kituwo 13-15, kinaitwa Albiidh, kituo 16-18 Dur’o kituo cha 19-21 kinaitwa Dhulum, kituwo 22-24 kinaitwa Hinas, kituwo 25-27 kinaitwa Daadi na kituwo cha mwisho 28-30 kinaitwa Muhaq.

 

Ndugu Muisilam hizi ndizo aya na viyuo zenye kuonesha sisi tuzingatiye sana hesabu za siku zetu kwa kutumiya mwezi sayari ili tupate Idadi na hesabu ya siku tunazozihitaji na vilevile tumepata fundisho lingine kuwa hapa MwenyeziMungu ameumba mwezi mmoja tu si zaidi ya mmoja kwa hiyo utakapoandama popote  pale ndipo hesabu zake zinapoanza na kuelekea katika vituo vyake kama Yeye Mwenyewe Alivyosema  kuwa Ameumba mwezisayari na Akaumba vituwo vyake.  Kutokana na mafundisho haya si dhani  kuwa mwezisayari utakapo onekana nchi ya mbali na nchi nyingine haikuuona kuwa eti vituo na hesabu zitatofautiana.  Kwa Mfano nchi hiyo iliyouona mwezisayari itakuwa tarehe moja kwao na nchi ya pili itakuwa wao bado wapo tarehe 29 au 30. Hili ni muhali halitewezekana kamwe katika maumbile ya MwenyeMungu ama katika mafundisho yake ya Qur-an kama tulivyoona aya za nyuma.

 

 Nini maana ya saumu

 

Kilugha saumu ni kujizuiya na kutenda kitu ambacho unaweza kukitenda au kujitowa katika hali fulani na ukajiweka katika hali nyingine, na mtu kiziwi anaitwa kwa kiarabu ”Assam” na anaambiwa aliye nyamaza  “saum” kwa kuwa kajizuiya na kuongeya  kama pale ilipotwambiya Qur an 

 

(…sema hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehma ya kufunga, kwa hiyo leo sitasema na mtu) Qur-ani19:26

 

Kisheriya saumu ni kujizuiya Mwisilam kula na kunywa na kumuingiliya mkeo kuanziya alfajir inapotoka mpaka juwa  linopozama na hiyo saum itatimia na kukamilika kama imeepukana na mambo yaliyoharamishwa.

 

Lini itafaradhishwa hii saum ya Ramadhani?

 

Saumu ya Ramadhan ilifaradhishishwa  tarehe 15 Shaaban mwaka wa 2 Hijiriya, na Mtume mwenyewe katika maisha yake kufunga Ramadhan 9 kauona mwezi kwa macho yake mara 2 kaletewa habari za mwezi mara 3 toka Madina na mara 4 toka nje, na akawa amefariki mwezi Rabii’al awal mwaka 11 Hijiriya,[s.a.w]

Dalili ya kufaradhishwa Mwezi wa Ramadhan

Saumu  ya Ramadhani imefaradhishwa kutoka ndani ya Qur-an na sunna sahihi ya Mtume  (s.a.w.).  Kasema MwenyeziMungu:

 (Enyi mlioamini mmelazimishwa kufunga saum) kama walivyolazimishwa  waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu )Qur-an 2:183.

Na katika sunna kasema Mtume (s.a.w.) {Uislam umejengeka katika nguzo tano kushuhudia ya kwamba hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mungu mmoja tu  ambaye ni Allah na Muhammadi ni Mtume wa Allah na kusimamisha sala(tano ). Na kutoa zaka na kufunga saum ya Ramadhani. Na kwenda kuhiji  kwa mwenye uwezo wa kwenda } Albukhari

Tunathibitisha vipi kuingiya kwa mwezi wa Ramadhani?

Kuingiya mwezi wa Ramadhani kunathibitishwa kwa njia 6 kuu.

1].kuona mwezisayari mtu peke yake itamlazimu nafsi yake afunge

2]Wakiona mwezisayari watu wengi itawalazimu watu wote wafunge

3] Wakiuona mwezisayari watu wachache na wakamueleza Kiongozi wa kiislaam itawalazimu watu wote wafunge.

4].Akiona mwezisayari mtu mmoja na akatowa habari kwa wengine katika eneo lina kiyongozi wa kiislam itawalazimu watu wote wafunge 

5.Akiona mwezisayari mtu mmoja na akatowa habari katika eneo lina Kiongozi wa kiislam lakini hashughulikii mambo ya waislam itawalaazimu watu wote wafunge.

6]Kuelekea katika mji ambao umeonekana kwao mwezisayari, tazama kitabu cha “Attalkhiss” kasema Imam Ibn hajar.

Dalili za kufunga Ramadhani kwa kuonekana mwezisayari popote pale duniyani

Waislam watawajibika kufunga Ramadhani kama utaonekana mwezisayari popote pale duniyani maadamu  tu uonekane huwo mwezisayari na  Mwislam hata kama aliyeuona ni mtu mmoja pasina kuweka kiwango cha msafa fulani, au kwenda kiwango cha  kutofautiyana machomozo ya mwezisayari, haya yote hayana dalili ndani ya mafundisho ya qur-an na sunna na hata Mtume (s.a.w.) aliyefaradhishiwa hii funga alipokuwa akiletewa taarifa ya kuonekana mwezisayari hakuwauliza waliomleteya habari hizo kuwa wanatokeya umbali gani au machomozo ya mwezi wao vipi, alikuwa akitosheka na ile taarifa ya kuonekana huo mwezisayari.  Wala hayakupatikana mafundisho kutoka kwa Mtume (s.a.w) aliwaambiya Waislam eti kila nchi ina muandamo wake. 

Wakati wa uhai wake nchi ya Yemeni na Sham zilishaingiya uislam na maeneo mengine mbalimbali uliingia uislam, hatukuona wala kusikia eti walikuwa wanatafutiana kufunga kama utakavyokuja  kuona mafundisho ya Mtume hapo mbele, na kama hawakuuona mwezisayari au hawakupata taarifa alikuwa akikamilisha Shaabani siku 30, haya ndiyo mafundisho ya Mtume   (s.a.w.).

 Na kuna hadith nyingi sana juu ya ibada hii ya funga tukianza na hadithi ya kwanza kasema Ibn Omar (R) katika hadithi alisimuliya ya kuwa (Aliuona mwezi na akamwambia Mtume (s.a.w.) kuwa ameona akafunga Mtume na akawaamrisha watu wote wafunge )[ Imepokewa na Abuu Dawdi na Ibn Hibban,]

Hapa tumeona kuwa Mtume (s.a.w.) ametosheka na taarifa ya mtu mmoja wala hakumuuliza umeonekana wapi na umbali gani.

Na kutoka kwa Rabii ibn Harash kutoka kwa mtu mmoja miyongoni mwa masahaba wa mtume (s.a.w)kasema:”

{Wamekhitalifiyana watu siku moja juu ya siku ya mwisho wa Ramadhani kuendelea kufunga au kufunguliya, wakaja mabedui wawili wakashuhudiya mbele ya Mtume (s.a.w.)kuwa wameona mwezi jana jiyoni, palepale akawaamrisha Mtume (s.a.w.)watu wafungulie} Ahmad na Abu Dawd

 

Vile vile  Mtume [s.a.w] hakuwauliza mbona sisi hatukuuona na mmetoka umbali gani au mbona machomozo yenu siyo sawa na sisi na kadhalika imekuja hadith kutoka kwa Abu Hurayra[R.A] Kasema Mtume: “ sumuu liruuyatihi, waaftiru liruuyatihi yaani  “Fungeni kwa kuonekana kwake[mwezi] na funguweni kwa kuonekana kwake”.

 

Hadith hii ni amri yenye kueneya kwa umma mzima  ilipotamkwa “suumuu” tamko hili linafidisha umuum katika qaida za usul fiqhi linaitwa “Al- Amru liljam-i biswighatil Jam-i”  tazama kitabu Irshadul Fuhuuli uk 121-122.

 

Na amesema Imam Ibn Qayyim  kuwa maneno yote anayosema Mtume [s.a.w] ni yenye kueneya kwa umma mzima madamu tu hakukusudiya kwa Fulani pekee.  Tukitazama hadith hiyo anasema Mtume tufunge utakapoonekana mwezi na siyo tutakapouona sisi ndiyo tufunge na kufunguwa bali utakapoonekana na waislamu popote pale ulimwenguni watu wafunge wala hakusema watu wa nchi Fulani wakiuona mwezi sayari haiwalazimu watu wa nchi nyingine kufunga. Kwani kama tulivyoona Mtume[s.a.w] yeye mwenyewe katika maisha yake kafunga Ramadhan 9 kauona mwezi mara 2 tu  mara 7 zote kaletewa taarifa.

 

Hoja na majibu kwa wale wanaohalalisha kuwa kila nchi ina machimbuko yake ya mwezi

 

Hoja yao kubwa siyo Quran wala Sunna ya Mtume[s.a.w] ambavyo ndiyo dira yetu tunapokhitilafiyana kama alivyosema Allah Taa’ala katika Qur an “… Na kama mkikhitilafiyana juu ya jambo lolote basi lirudisheni kwa MwenyeziMungu na Mtume, ikiwa mnamuamini MwenyeziMungu na siku ya mwisho, hiyo ndiyo kheri nayo ina matokeo bora kabisa[Qur 4:59]

 

Hoja kubwa ya wenye kuhalalisha kila nchi kuwa na mwezi wake ni moja tu nayo ni kisa cha Kuraybu mtumwa wa Ibn Abas walipojadiliyana na Ibn Abas mwenyewe anasema Kuraybu kuwa Ummullfudhli binty Harith [mama yake huyu Ibn Abasi] alinituma kwa Muawiyya katika mji wa Shamu nikafika Shamu na kutekeleza haja zake [zote]na ukaonekana mwezisayari wa mwezi wa Ramadhan, na mimi nipo Shamu, tukauona mwezisayari usiku wa kuamkiya Ijumaa, baada ya hapo nikarudi Madina mwisho wa mwezi [wa Ramadhan] akaniuliza  Ibn Abas, kisha akautaja mwezi akasema : lini mliuona mwezi? nikamwambiya usiku wa kuamkiya Ijumaa. Akasema kuniuliza wewe umeuona usiku wa kuamkiya Ijumaa? Nikajibu ndiyo na wameuona watu [wote] na wakafunga, na akafunga Muawiyya [piya] akasema Ibn Abas lakini sisi tumeuona mwezi usiku wa kuamkiya Jumamosi na tutaendeleya kufunga mpaka tukamilishe siku 30, au tuuone[wenyewe], nikamwambiya [Ibn Abas] je hukutosheka kwa kuuona Muawiyya na kufunga kwake akajibu kwa kusema hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume [s.a.w].

 

Ndugu waislamu hii ndiyo dalili kubwa ya wenye kuhalalisha kila nchi kuwa na mwezi mwandamo wake kwa hakika hawana dalili nyingine zaidi ya kisa hiki, hebu tukichambuwe kwa undani sote ili kila mmoja wetu apate faida je kinafaa kuwa ni dalili ya kutegemeya?

 

Kumjadili Kuraybu na uchambuzi wa  kisa hiki

 

Kwanza watukufu waislamu kabla hatujasogeya kwenda mbali inabidi mpate faida kumjuwa huyu Kuraybu ni nani? Hili jina la Kuraybu ni la baba yake ambaye na wanachuwoni wa hadith wanamkubali huyu baba yake kuwa alikuwa mtu mkweli sana na anategemewa katika upokezi wa hadith tazama kitabu  'Tahdhibu'  cha Imam Ibn Hajar Al Asqalani [ jalada la 3 uk 468 chapa ya Beurut tazama mahala pa herufi kafu]

 

Na tazama vile katika Taqribu Tahdhibu cha huyu huyu Ibn Hajar Al Asqalani jalada la 2uk 28. lakini huyu aliye katika kadhiya hii na Ibn Abas jina lake kamili ni Muhamad Ibn Kureybu Ibn Abi Muslim  AL Hashimiy alikuwa ni mtumwa wa  Ibn Abasi na mama yake Ibn Abasi UmulFadhli alikuwa akimtuma sana kwenda Shamu kwa Muawiyya.

 

 Na yeye huyu si Sahaba bali ni katika tabiin na si mtu kuaminika katika elimu ya hadith hakubaliki. Hebu tuwasikilize wanachuwoni wetu wa hadith wanavyomchambuwa huyu Muhamad Bin Kuraybu.

 

Amesema Athram toka kwa Ahmad bin Hanbal kuwa "huyu Muhammad Bin Kuraybu hadith zake ni 'Munkar'"  Na amesema Ad Duuriyu toka kwa Ibn Maiyn kuwa "hadith zake huyu si chochote". Na amesema Ibn Numair; "upokezi wake haufai kabisa ni dhaifu".  Na amesema Ibn Hatim toka kwa baba yake kuwa "Huyu Muhamad Bin Kureybu hazitolewi hoja hadith zake".  Na  amesema Abi Zur’a kuwa "Hadith zake ni laini mno".  Na amesema  Imam Bukhar kuwa "Hadith zake huyu ni za kuchunguzwa sana". Na akaendeleya kusema Imam Bukhari kuwa "Hadith zake huyu ni Munkar hazikubaliki".

 

Kumbuka ndugu Muislamu pindi imam Bukhar anaposema kuwa hadith za mtu Fulani ni munkar basi wanachuwoni wote wa hadith wamekubaliyana kuwa zinawekwa upande wa dhaifu.

Na amesema Imam Nnasai "Huyu Muhamad Ibn Kureybu ni dhaifu". NA vivyo amesema Imam Adar qutni [Tamaza Tah-dhibu Tah-dhibu ya Imam Ibn Hajar AL Asqalani jalada la 3 uk 684-685 chapa ya Beirut.  Tazama mahala pa herufi mimu ] piya Taqribu Tah-dhibu jalada la 2 ukurasa 86.  Na amesema  Abubakar Al Athram: "Nilimuuliza Imam Ahmad Bin Anmbal kuhusiyana na hadith za huyu Muhamad Bin Kuraibu akasema 'Ni Munkar kwa sababu analeta hadith za ajabu kabisa". [tazama Al Jarhu Wataadil cha Imam Ibn Abi Hatim jalada la 8 uk.68chapa ya Indiya]

 

Na amesema Imam Ibn Hiban kama alivyonukuliwa katika Mizanul i’tidali ya Dhahabi kuwa "Huyu Muhamad bin Kureybu alikuwa ni mudalisi[mrongo]". Na amesema Abu Na’im Ad Damishq kuwa,  "Huyu Muhamd Bin Kureybu alikuwa anachanganya hadith sahihi na dhaifu". 

 

Kkumbuka ndugu muislamu hakuna hata mwanachuwoni mmoja wa hadith aliyemtaja huyu Muhamad Ibn Kureybu kuwa ni mkweli.

 

Baada ya kumaliza kumkaguwa huyu Kureybu  ebu sasa ndugu Muislamu tuje kukikaguwa kisa chenyewe , tukianza na qauli ya Ibn Abas kukataa kufunguliya kwa mwezi ulioonekana katika mji wa Shamu kasema Imam Alqarafi katika kitabu cha “Adhakhira” ya kuwa,  "Siku ile  habari ya mwezi alipopewa Ibn Abas kutoka kwa Kureybu kulikuwa hakuna mawingu yaliyotandaa katika mji wa Madina, na wala haukuonekana mwezi siku hiyo , Ibn Abas akatanguliza kuuona yeye mwezi kuliko ile habari  au taarifa alioletewa na Kureybu, na ndiyo maana akasema : hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume[s.a.w] Kwa maana tusichukuwe habari za dhana na tukaacha yakini, japokuwa hakuna tafauti ya kuutazamiya mwezi kukiwa kuna mawingu au hakuna mawingu, lakini yeye alihukumu kwa kuuona  mwezi.  Anasema Imam Alqarafi kuwa "Hiki kisa kishakuwa na  na utata mkubwa"  tazama J. 2 uk 490.

 

Na qauli ya Ibn Abas ya kukataa kufunguliya mwezi ulioonekana Shamu na kusema hivi ndivyo alivyotuamrisha Mtume[s.a.w] na akaishiya hapo hakuendeleya na wala hakufafanuwa zaidi na kisa hiki kikaishiya hapo. Na utata ukawa mkubwa katika safu za Waislamu kutokana na kutokupatikana ufafanuzi zaidi juu ya kisa hiki. 

 

Sasa basi tujiulize sote kwa pamoja kaamrishwa na Mtume[s.a.w] nini? Wamekhitilafiyana wanazuwoni katika makundi manane juu ya hii amri anayosema Ibn Abas kaamrishwa na  Mtume[s.a.w]

 

1)   Kundi la kwanza la wanazuwoni wanasema kaamrishwa na Mtume [s.a.w] asifunge wala kufunguwa katika siku itakayokuwa mawingu yametanda angani wakamilishe 30 shaaban au 30 Ramadhan

 

2)   Kundi la pili wao wanasema: kaamrishwa na Mtume[s.a.w] asipokee taarifa ya kufunga   au kufunguwa kutoka kwa mtumwa kwa sababu wale wote walioleta habari ya mwezi wa kufunga au kufunguwa  zama za Mtume [s.a.w] walikuwa si watumwa, na Kureybu alikuwa ni mtumwa wa Ibn Abas [r.a]

 

 

3)   Kundi la tatu wao wanasema kaamrishwa na Mtume[s.a.w] asipokee taarifa au habari ya mwezi kutoka kwa mtu mmoja tu mpaka apatikane mwingine mwenye kumshuhudiya huyo mtowa habari.

 

4)   Kundi la nne wanasema kaamrishwa na Mtume [s.a.w]  kwa yeyote yule atakaye safiri kutoka katika mji ambao haukuonekana mwezi na kuelekeya katika mji ambao umeonekana, basi hukumu yake atafunga pamoja na watu wa mji huo na atakuwa ni mmoja kati ya watu wa mji huwo. Kwa mujibu ya mafundisho haya ya Kureybu, atatakiwa afunge siku 31.

 

 

5)   Kundi la tano wao wamesema kaamrishwa na Mtume[s.a.w] asikubali mwezi aliyouona Muawiyya kwa sababu mtazamo wake yeye Ibn Abas[r.a.] alikuwa hautambui utawala wa Muawiyya na alisimama pamoja na Ally bin Abi Twalibu dhidi ya Muawiyya. Kwa mafundisho haya asikubali mwezi ulioonekana na kiyongozi asiyetambulika.

 

6)   Kundi la sita wamesema kaamrishwa na Mtume [s.a.w] asikubali kufunguwa na kulipa siku badala yake ile waliokula mchana na isipokuwa kwa mashahidi wawili kwa hilo kuhofiya kuwalipisha watu funga ya siku moja iliyowapita kutokana na taarifa ya mtu mmoja.

 

 

7)   Kundi la saba wanasema kaamrishwa na Mtume [s.a.w] kila nchi ina machomozo ya mwezisayari wake na masafa yake, na masafa yanayokusudiwa ni KM.133.056.

 

QAULI YA MADHEHEBU MANNE JUU YA QADHIYA HII

 

Ndugu Muislamu kuna madai ya uwongo kabisa yaliyozoeleka midomoni mwa baadhi ya ndugu zetu kuwa eti wanazuwoni wengi wamesema kila nchi ifunge kwa machomozo ya  mwezi wake wasitegemee machomozo ya wenzao. Qauli hii si sahihi kabisa. Kwa kweli mwenye kueneza qauli ya namna hii  hana uaminifu katika elimu kwani anaeneza qauli ya upande mmoja ambao ambao ndiyo mtazamo wake yeye na anaficha huja za upande mwingine. Tafadhali mpendwa Muislamu ebu soma kwa makini  tunataja misimamo ya madhehebu manne na wewe mwenyewe pima kwa akili yako bila matamaniyo ya nafsi au ushabiki je wanazuwoni wengi wapi wameegemeya:

 

a)   Tukianza na wanazuwoni wa ki-Hanafi wao wanasema: "Kutafautiyana kwa machomozo ya mwezi haizingatiwi katika madhehebu yetu, na ndiyo wanazuwoni wengi walikwenda hivi, na hii ndiyo fatwa yetu, inawalazimu watu mashariki kufunga kwa kuonekana mwezi na watu wa Magharibi kama itathibiti kwao wameuona huo mwezi, kwa njiya za kisheriya".

 

b)   Wanazuwoni wa Ki-Maliki wao wanasema: "Utakapoonekana mwezi, itaeneya uwajibu wa kufunga nchi zote, iwe nchi hiyo ya karibu au mbali, wala haizingatiwi katika hilo umbali wa masafa, na vile vile haitazingatiwa kuwafikya machomozo au kutafautiyana machomozo, wajibu kufunga kila atakaeletewa taarifa ya kuonekana mwezi wawe walioleta taarifa hiyo, mashahidi wawili au watu wachache au hata watu wengi."

 

 

c)    Wanazuwoni wa Ki-Hanbal wao wamesema "Iitakapotihibiti kuonekana kwa mwezi sehemu Fulani, iwe karibu au mbali, italazimu watu wote wafunge , na hukumu ya wasiouona ni hukumu ya waliouona".

 

d)   Wanazuwoni wa Ki-Shafi’i wao wamesema: "Utakapoonekana mwezi katika mji itawalazimu hukumu ya kufunga watu wa mji wa karibu si watu wa mbali kwa kadiri ya  tafauti yao ya machomozo ya mwezi, na tafauti ya machomozo kati ya sehemu moja na nyingine isipunguwe chini ya Farsakh 24 sawa sawa na kama KM 133.056".

 

Kwa maana hiyo nchi kama ya Tanzaniya ina mikowa 26 na kutoka mkowa mmoja kwenda mwingine haiupunguwi chini ya KM 200 kama tutafuwata madhehebu haya ya Kishafi’I itabidi katika mikowa 26 kila mkowa utakuwa na funga yake.  Kwa mfano Dar es salaam kwenda Morogoro ni kilo KM.198 hawa watakuwa wamevuka kiwango cha kufunga pamoja kwa kipimo cha madhehebu ya Kishafi’I ambacho ni KM 133.056, kwa maana hiyo Morogoro wao watafunga pamoja na watu wa Kibaha kwa kuwa masafa kati ya Morogoro na Kibaha ni KM 148 takriban. Sasa je ndugu Muislamu hili linawezekana na linaingiya akilini? Mpendwa Muislamu tumiya akili yako kujadili hoja hizo maana wewe mwenyewe ndiye utaulizwa kesho akhera na si sheikh Fulani au Imamu

 

Wabillah Tawfiiq Waswalallahu ala Muhammad waala ali Muhamad

 

Kama una hujja yoyote au maswali basi tuandikiye

 

Vijana wa Salafiyya

Box 16101 Dar es salaam

Lukwati @yahoo.co.uk