|
Anasema
Allaah
سبحانه وتعالى
}}يَا
أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا
كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ{{
}}
أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَى
سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ وَعَلَى الَّذِينَ
يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا
فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ وَأَن تَصُومُواْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ
تَعْلَمُونَ{{
}}
شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ
وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ
الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ
فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ
وَلاَ يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُواْ الْعِدَّةَ
وَلِتُكَبِّرُواْ اللّهَ عَلَى مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ
تَشْكُرُونَ{{
{{Enyi
mlio amini! Mmeandikiwa Saumu, kama waliyo andikiwa walio kuwa kabla
yenu ili mpate kuchamngu}}
{{(Mfunge) siku maalumu za kuhisabika. Na atakaye kuwa miongoni
mwenu mgonjwa au yumo safarini basi atimize hisabu katika siku
nyengine. Na wale wasio weza, watoe fidiya kwa kumlisha masikini. Na
atakaye fanya wema kwa kujitolea, basi ni bora kwake. Na mkifunga ni
bora kwenu, kama mnajua}}
{{Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa ni
uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi.
Basi ataye kuwa mjini katika mwezi huu naafunge. Na mwenye kuwa
mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine.
Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo
mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa
amekuongoeni ili mpate kushukuru}}
Al-Baqarah: 183-185
Inaputasa
tumshukuru Allaah
سبحانه وتعالى
kwa Kutujaalia uhai na afya mpaka tunakaribia kufika mwezi mtuku wa
Ramadhaan na hii ni fursa nyingine Anayotupa katika maisha yetu
kushuhudia mwezi huu na kupata fadhila zake.
Na hii ni
neema ya Allaah
سبحانه وتعالى Ambaye
Ametujaalia kuwa na miezi iliyo bora kuliko miezi mingine au siku
bora au masaa bora kuliko mengine, ambazo thawabu zake za mema
yanayotendeka humo huwa ni zaidi ya nyakati nyingine. Mfano wake ni
kama kunapokuwa na SALE dukani, ambayo kawaida yake huwekwa muda
mdogo tu. Na muda huu mtu huweza kununua vitu vingi kwa malipo
kidogo tu. Hali kadhalika Ramadhaan, ni mwezi mmoja tu, lakini
malipo yake huwa ni mengi kuliko hata malipo ya miezi yote
mingine. Ikiwa mtu atatimiza Swawm yake inavyopaswa na kufanya mema
mengi, na akawa katika Twa'a kamili na kuomba maghfira, basi hutoka
katika mwezi huu akiwa ameghufuriwa madhambi yake. Amesema Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
((
من صام رمضان إيماناً واحتساباً ، غفر له ما تقدم من ذنبه ))
أخرجه البخاري ومسلم
((Atakayefunga
Ramadhaan kwa imaani na kutaraji malipo, ataghufuriwa madhambi yake
yaliyotangulia)) Al-Bukhariy
na Muslim
Ramadhaan ni
mwezi ambao tunatimiza Fardhi mojawapo ya Kiislamu. Ni mwezi uliojaa
baraka, kheri na rahma za Allaah
سبحانه وتعالى. Kila
Muislamu inampasa aukaribishe mwezi huu kwa furaha na matumaini
kamili.
Zifuatazo ni njia
kumi za kujitayarisha kuukaribisha mwezi wa Ramadhaan na kupata
manufaa makubwa pindi utakapotimiza:
1.
Du'aa
Anza kwa kuomba
Du'aa kwamba mwezi huu ukufikie wakati umo katika hali ya siha nzuri
na usalama hata uweze kufunga na kufanya ibada zako kwa hamu kubwa na wepesi.
((عن
أنس بن مالك رضي الله ع أنه
قال كان النبي صلى الله عليه وسلم إذا دخل رجب قال: اللهم بارك لنا في
رجب
وشعبان وبلغنا رمضان)) رواه
أحمد والطبراني
((Imetoka kwa Anas Bin
Maalik
رضي الله عنه
kwamba unapoingia mwezi wa Rajab, Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alikuwa akisema: Ya Allaah tubarikie Rajab na Shaaban na tufikishe
Ramadhaan)) Ahmad na
At-Tabariy
Na anapouona mwezi
wa Ramadhaan husema:
((اللهُ أَكْـبَر، اللّهُمَّ أَهِلَّـهُ عَلَيْـنا
بِالأمْـنِ وَالإيمـان، والسَّلامَـةِ والإسْلامِ، وَالتَّـوْفيـقِ
لِما
تُحِـبُّ
وَتَـرَْضى،
رَبُّنـا وَرَبُّكَ اللهُ ))
رواه الترمذي
والدارمي وصححه ابن حبان
.
((Mwenyezi
Mungu ni Mkubwa, Ewe Mwenyezi Mungu Uanzishe kwetu kwa amani na
imani, na usalama na Uislamu, na tawfiq ya kile Unachokipenda Mola
wetu na Kukiridhia, Mola wetu na Mola wako ni Mwenyezi Mungu))
At-Tirmidhy, Ad-Daraamiy na
kasahihisha Ibn Hibbaan
2.
Mazoezi katika
mwezi wa Sha'baan
Funga Sunnah
nyingi katika mwezi wa Sha'abaan, soma Qur'aan Juzuu moja kila siku
au chini yake, amka usiku uswali japo Raka'a mbili, kisha zidisha
kidogo kidogo hadi inapoingia Ramadhaan uwe tayari umeshapata
mazoezi mazuri.
3.
Shukurani
Mshukuru
Allaah
سبحانه وتعالى
Kukupa uhai na siha hata uifikie Ramadhaan nyingine.
Imaam An-Nawawy alisema, kwamba shukurani
inapasa kwa kila jambo jema unalojaaliwa kubwa au dogo na vile vile
shukurani inapasa kwa kila jambo baya Analokuepusha nalo Allaah
سبحانه وتعالى.
Kwa hivyo fanya 'Sajdatus-Shukur' kwa neema hii tukufu.
4.
Furaha
Furahia
kukufikia mwezi wa Ramdhaan kama unavyomfurahikia mgeni mpenzi
anapokuja kwako na kumuandalia mazuri yote. Maswahaaba (Mwenyeezi
Mungu Awe radhi nao), walikuwa
wakiamkiana unapoingia mwezi wa Ramadhaan na Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alikuwa akisema hivi anapowapa habari nzuri za mwezi wa Ramadhaan:
((جاءكم شهر مبارك افترض عليكم
صيامه تفتح فيه أبواب الجنة وتغلق فيه أبواب
الجحيم وتغل فيه الشياطين
فيه
ليلة خير من ألف شهر من حرم خيرها فقد حرم))
رواه أحمد
((Umekujieni mwezi wa
Ramadhaan, ni mwezi wa Baraka. Imefanywa Swawm kwenu kuwa ni Fardh,
milango ya Pepo hufunguliwa na milango ya moto hufungwa na
mashaytaan hufungwa. Umo katika mwezi huu usiku ulio bora kuliko
miezi alfu. Atakayenyimwa kheri zake
hakika
kanyimwa)) Ahmad
5. Jipangie
wakati na weka maazimio
Ni jambo la
kusikitisha kuona watu wengi wanafurahia mwezi wa Ramadhaan na
kupanga mambo ya kidunia badala ya mambo ya Akhera. Wengi
hukimbilia kwenda sokoni kununua nguo za 'Iyd, na kufurahikia
vipindi vya Ramadhaani katika televisheni ambavyo sio vya dini
kama 'silsilal' (maonyesho ya sinema yanayoendelea), au kucheza
karata, dhumna, au kukutana barazani na kupiga gumzo na kadhalika,
hali ambapo huu ni mwezi wa kufanya ibaada na fursa ya kujichumia
mema mengi yamfaayo mtu Akhera. Kwa hiyo ndugu Waislamu, tujitahidi
kuutumia wakati wetu wote bila ya kupoteza hata dakika moja, na
muhimu sana kujipangia mapema wakati wako kama ifuatavyo:
·
Ni bora
kujipangia nyakati zote za mwezi mzima vipi utatumia muda wako wa
mchana na usiku. Weka 'azma ya dhati kuchukua fursa kamili ya wakati
wote wa mwezi huu.
·
Weka mpango
ma'aluum wa kazi zako hata uweze kuswali kwa wakati kila kipindi,
kusoma Qur'aan, kula daku na mengineyo kama tutakavyotaja hapa
chini.
·
Kama ni
mwanafunzi na kama unakuwa ukisoma usiku, lala mapema, kisha uamke
uswali Qiyaamul-Llayl na usome masomo yako baada ya hapo.
·
Anza mpango wako
kwa siku chache na kama unahitaji kurekebisha kuboresha nidhaam yako
fanya hivyo uweze kujua nidhaam ipi inayowafikiana na hali yako.
·
Nasiha
kwa kina Dada:
Msipoteze
muda mwingi jikoni kwa kuanda vyakula vingi
kisha hata visiliwe vyote,
mkaingia katika israaf. Na wakati mko jikoni mtajeni Allaah
سبحانه وتعالى
huku mnafanya kazi zenu, kwa Dhikr na Tasbiyh,
kwa hali hiyo mtaweza kupata
thawabu za kupika na kumkumbuka Allaah
سبحانه وتعالى
kwa wakati mmoja.
6. Tawbah
na Maghfirah
Omba Tawbah
Nasuuha kwa Mola wako na waombe msamaha wale uliowakosea. Kufanya
hivi kutanufaisha zaidi Swawm na Swalah zako na pia kukupa imani
kuwa huna haki ya mtu.
7.
Jifunze Fiqhi ya Swaum
Jifunze
elimu ya mambo yanayohusu Swawm (Fiqhi ya funga), hiyo ni muhimu ili
usije kufanya jambo la kuharibu Swawm yako. Jifunze Swawm kama
aliyokuwa akifunga Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
ndio mfano bora kabisa wa kuufuata.
Swawm
haifunguliwi kwa kula na kunywa tu, bali pia ni kujiepusha na maneno
mabaya na kufanya mambo mabaya kama kusengenya, kutukana, kugombana.
Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
amesema:
((من
لم يدع قول الزور والعمل به والجهل فليس لله حاجة في أن يدع
طعامه وشرابه)) البخاري
((Yeyote asiyeacha
kusema maneno mabaya? Na vitendo vibaya basi hana haja kuacha
chakula chake na maji))
Al-Bukhariy
7.
Jitayarishe kuchuma mema mengi
:
Mwezi wa Ramadhaan
ni mwezi wa ukarimu, huruma Rahma na mapenzi.
· Panga
kabisa na kuweka kiwango fulani cha kutoa Sadaka na kutoa kwa
maskini, anzia kwanza kwa ndugu, jamaa.
· Kama
inakupasa kutoa Zakah, na umependa iwe katika mwezi wa Ramadhaan
fanya hima uitimize Fardhi hii pia.
· Weka
'azma ya kufuturisha kwa kualika ndugu, jamaa, jirani na marafiki
kwani kumfuturisha mtu ni thawabu.
((قال صلى الله عليه وسلم : من فطر صائماً كان له
مثل أجره غير أنه لا ينقص من
أجر الصائم شيء ))
أخرجه
أحمد والنسائي وصححه الألبان
((Amesema Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
"Atakayemfuturisha aliyefunga, atapata ujira kama ujira wake bila ya
kupungua chochote katika ujira wa yule aliyefunga))
Ahmad, An-Nasaaiy na kasahihisha Sh
Albani
· Kama
unaye jirani asiye Muislamu, mjulishe kuhusu Ramadhaan, faida na
Fadhila zake. Hii ni njia na fursa mojawapo ya kufanya da'awah
kwa jirani yako.
8.
Hitimisha Qur'aan, Hifadhi na
jifunze Tarjama
Jipangie
wakati uweze kuhitimisha Qur'aan kwani Ramadhaan ndio mwezi
ulioteremshwa Qur'aan na hii ni Sunnah aliyokuwa akifanya Jibriyl
عليه السلام
kwa Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
kusoma naye Qur'aan yote
((عن ابن عباس رضي الله عنهما قال: "كان رسول
الله صلى الله عليه وسلم أجود الناس، وكان
أجود ما يكون
في رمضان حين يلقاه
جبريل، وكان يلقاه في كل ليلة من رمضان فيدارسه
القرآن؛ فلَرسول الله صلى الله
عليه
وسلم أجود بالخير من الريح المرسلة ((رواه
البخاري ومسلم
((Kutoka kwa Ibn
'Abbaas
رضي الله عنهما
kwamba
Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
alikuwa ni
mbora (mwenye matendo mema) wa watu, lakini alikuwa mbora zaidi
katika Ramadhaan wakati Jibriyl anapokutana naye, na alikuwa
anakutana naye kila usiku wa Ramadhaan akimfundisha Qur'aan na Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم
ni mbora wa
kheri kuliko upepo uanovuma)) Al-Bukhariy
na Muslim
Katika muda wa
masaa 24 weka saa moja au mbili khaswa iwe ya Qur'aan kusoma na
kujifunza maana ya maneno ya Mola wako uonje ladha ya Qur'aan. Vile
vile jitahidi kujiwekea wakati wa kuhifadhi japo sura ndogo ili
ukitoka katika Ramadhaani uwe una sura zaidi za kusoma katika Swalah
zako.
9.
Darsa
Hudhuria
Darsa katika mwezi huu au soma vitabu vya dini, au sikiliza
mawaidha. Jambo hili ni muhimu sana kwani kusikiliza mawaidha ni
njia muhimu na bora kabisa katika kuzidisha imani yako. Kwa hakika
unahitaji saa tu kuweza kutimiza jambo hili muhimu kila siku. Kama
huwezi kuhudhuria msikitini,
Alhamdulillah, TAWHIYD.CO.UK
imewatayarishia mawaidha mengi ya kusikiliza na ya VIDEO. Kwa hiyo
badala ya kutazama televisheni na kusikiliza muziki jambo ambalo ni
haramu ni bora utazame na kusikiliza mawaidha ujipate manufaa.
Kumbuka kwamba kama vile
mwili unavyohitajia chakula,
hali kadhalika Moyo na Nafsi zinahitaji chakula chake nacho ni
kumkumbuka Allaah سبحانه وتعالى kwa
kila aina ya ukumbusho, na mawaidha ni mojawapo wa chakula kizuri
kabisa cha kutakasa Moyo na Nafsi kwa kuzijaza imaan na mapenzi ya
Mola Wako Mtukufu.
10.
Fungua 'Swafha' (Ukurasa) mpya katika maisha yako
Baada ya
kuweza kuyatimiza hayo yote, bila ya shaka hali yako ya imani
imekuwa bora kabisa na utakuwa umejibadilisha na kuwa mtu tofauti na
ulivyo. Kwa hivyo weka 'azma ya kuendelea hata baada ya Ramadhaan
kuwa katika twa'a na ibada, na kuendeleza Qiyaamul-Layl (Swalah ya
usiku),kusoma Qur'aan japo kidogo KILA
SIKU, na iwe umefungua UKURASA MPYA wa maisha yako na kumuomba
Allaah
سبحانه
وتعالى
Akuendeleze katika hali hii.
Tunachukua Fursa
hii ya kuwaombeeni Ramadhaan yenye baraka na kheri nyingi, tutoke
katika mwezi huu tukiwa tumesafishwa madhambi yetu yote, na wenye
kubeba thawabu nyingi ziwe nzito katika Miyzaan ya Hasanaat siku ya
Qiyaamah.
اللَّهُمَّ تَقَبَّلْ مِنّأ وَ مِنْكُم صَالح الأّعْماَل
Allaahumma Taqabbal Minnaa wa Minkum Swaalih al-A'aamal.
Aamiyn
|