Mtume
wa Mwenyezi Mungu (SA.W) alipata watoto sita kutokana
na mkewe wa mwanzo Bibi Khadija binti Khuwaylid (RA), wanaume wawili na wanawake
wanne. Watoto wa kiume aliwapa majina ya Qassim na
Abdullah aliyekuwa akijulikana pia kwa jina la Al Taher, amma watoto wa kike ni
Zeinab na Ruqayyah na Ummu Kulthum na Fatima (RA).
(Zipo riwaya
zinazosema kuwa alitangulia Fatima (RA) kisha Ruqayah (RA)
na nyingine zinasema kinyume na hiyvo).
Qassim aliyezaliwa
katika mwaka wao wa mwanzo wa kuoana alifariki dunia
akiwa na umri wa miaka miwili, na kutokana naye Mtume wa Mwenyezi Mungu (SAW)
anakajulikana kwa jina la ‘Abal Qassim’, yaani babake Qassim.
Kisha akazaliwa Abdullah
aliyefariki pia akiwa mtoto mchanga, kisha Zeinab, kisha Ruqayah aliyefanana
sana
na mama yake, kisha akazaliwa Ummu Kulthum, kisha akazaliwa
Fatima
aliyefanana
sana
na baba yake, hasa katika mwendo na sauti.
Katika mafulululizo
wa makala haya nitaeleza kwa ufupi juu ya maisha ya mabinti wane wa Mtume wa
Mwenyezi Mungu (SAW), nikianzia na mkubwa wao kwa umri, Bibi Zeinab, kisha Bibi
Ummu Kulthum kisha Bibi Ruqayyah na mwisho Bibi Fatima – Mwenyezi Mungu awe
radhi nao wote kwa pamoja.