TAWHIYD
    Tawhiyd

Qur'aan

Sunnah

Fiqhi

Makala

Nasiha Ya Ijumaa

Dua na Adhkaar

'Aqiyda-Tawhiyd

Vitabu

Darsa za Wanawake

    Sikiliza

Qur'aan

Mawaidha

Dua

Nashiyd

    Tizama

Video

 » Sunnah  

YALIYOKUWA SUNNAH NA YALIYOKUWA BID’AH

 KATIKA SHEREHE ZA ‘IYD

Imefasiriwa na Umu 'Abdul-Wahaab

“Kwa kila jamii ya watu kuna sikukuu, na hii ‘Iyd ndiyo sikukuu yetu” alisema Mtume (s.a.w) kumwambia Abu Bakr (r.a). [Al Bukhaariy na Muslim].

“Sikukuu yetu” ina maana kubwa kwa Waislaam, kwa sababu  inatujulisha kwamba hii ni yetu na asili yake imetokea kwenye sharia zetu tu  peke yake.  Kwa kuwa sherehe hizi zimeegemea kwenye taratibu za kidini, ni muhimu sana kuzifafanua ili ziwe na furaha kubwa na mikusanyiko yenye kuleta hisia ya kuwa hizi sikukuu ni zetu (sisi Waislaam), na ni tofauti na zile sikukuu za Mushrikina. Haturuhusiwi kusherehekea Christmas, Hanuka, au sikukuu za Kipagani, na shukrani zetu zote tuzielekeze kwa Allaah (s.w.t) peke yake.

Mtume (s.a.w) ametuamrisha katika hutuba zake nyingi kuwa tujitofautishe na Mushrikin (Wapagani), na hizi ‘Iyd mbili ni miongoni mwa sikukuu zile ambazo Mtume (s.a.w) ametutaka tuchukue tahadhari kubwa ya kujitofautisha sana nao (Mushrikin).  Ndiyo sababu akasema, baada ya kuona watu wa Madinah walipokuwa na sherehe mbili wakizisherehekea kabla ya kuja Uislaam, “Allaah (s.w.t) ameshakupeni nyinyi kilicho bora kuliko vyote (sikukuu):  ‘Iyd-l-Adh-haa (ya kuchinja) na ‘Iyd-l-Fitr”. [Ahmad, Abu Dawuud na An Nasaa’iy].

 ‘Iyd-l-Adhaa huja baada ya kumalizika ibada ya Hijja na ‘Iyd-l-Fitr huja baada ya kumalizika saumu ya mwezi wa Ramadhani. Kwa hivyo haishangazi hiyo, ni lazima tuzionyeshe na tuzifafanue  ‘Iyd zetu. Kutokana na bayana hizi zilizo wazi, Wanavyuoni wa Kiislaam ni lazima watilie mkazo sana juu ya kuzitofautisha sherehe zetu kutokana na zile za Mushrikin.

Hii ni kwa sababu sherehe zina taathira kubwa katika akili na tabia ya mwanaadam. Kuwa tofauti katika Sherehe vile vile ina maana kwamba ni lazima tusijishirikishe (tusihudhurie) kabisa katika sherehe za Mushrikin. ‘Umar (r.a) amesema: “Msijifundishe lugha ya Mushrikin – bila ya kuwa kuna umuhimu ndani yake – wala Msiingie makanisani wakati wa sherehe zao kwa sababu Hasira za Allaah huteremka juu yao.” [Al Bayhaqiy].

 

Sisi, Waislaam, huenda hata tufunge (saumu) katika siku za sikukuu za Mushrikin. Umm Salamah (r.a) amesema Mtume (s.a.w) alikuwa na kawaida ya kufunga siku za Jumamosi na Jumapili, na alipoulizwa Alisema: Kuna siku mbili katika siku za sherehe za Mushrikin kwa hivyo napenda kwenda kinyume na wao katika sherehe zao”. [Ahmad na An Nasaaiy].    

Kulikadiria wazo hili la kuwa tofauti na Mushrikin, ni muhimu sana kusema kwamba: Ili tuwe tofauti kwenye sherehe zetu na katika mwenendo ambao Mtume (s.a.w) ametutaka tuwe nao, ni lazima tufuate mwenendo wake (Sunnah) kikamilifu. Kwa kufanya hivyo kutatupatia malipo mema (thawabu) ya kuwa wafuasi wa kweli wa Mtume (s.a.w).

Kwa hivyo tukitaka kuwa wafuasi wake ni lazima tuelewe ni yepi Bid’ah (uzushi) katika sherehe zetu. Bid’ah inakuja pale Sunnah hutumika mahali pasipo pake! Ibn Taymiyyah amesema: “ Hakuna nafasi katika moyo wa binaadam kwa yote mawili; Sunnah na Bid’ah.” [Al-Iqtidhaa]. Allaah (s.w.t) amesema:

{Sema – Ewe Muhammad – Ikiwa kweli mnampenda Allaah basi nifuateni mimi, Allaah Atakupendeni}. [Aali-Imraan, 3:31]

Ndugu wapenzi, tunawasilisha kwenu baadhi ya matendo ya Sunnah katika sikukuu ili muweze kujaribu kuyatekeleza. Vile vile yanawasilishwa baadhi ya yaliyokuwa Bid’ah ili katika sikukuu muweze kuyaepuka. Kuna umuhimu mkubwa sana katika kufuata mwenendo wa Mtume (s.a.w) wa ‘Iyd ili kikweli kweli tuweze kusema kwamba sikukuu zetu ni tofauti na zile sikukuu za Mushrikin.

Yaliyokuwa Sunnah Katika ‘Iyd

1)     Siku ya ‘Iyd ni Sunnah kuvaa mavazi mazuri kabisa tuliyo nayo. Imehadithiwa kwamba Ibn ‘Umar alikuwa akifanya hivyo pamoja na Masahaba wa Mtume (s.a.w). [Fath al-Bariy] 

2)    Ni lazima (Waajib) kusali Salaa ya ‘Iyd-l-Fitr. Mtume (s.a.w) na Masahaba zake hawakuacha kabisa kufanya hivyo, na vile vile walikuwa wakiwakusanya watu kuitekeleza Salaa hiyo wakiwemo wanawake wenye  hedhi (hawaingii kwenye kusali lakini wanashuhudia kheri na du’a kwa Waislamu), watoto na vikongwe. [Al Bukhaary na Muslim].

3)     Ni Sunnah kula tende kabla ya kuondoka kuelekea kusali Salaa ya ‘Iyd ili kuonyesha kwamba hatujafunga. “Mtume (s.a.w) alikuwa hatoki kwenda kusali Salaa ya ‘Iyd ila baada ya kula tende.” [Al Bukhariy na Ahmad].

4)       Ni Sunnah kuleta Takbira kwa sauti tunapotoka majumbani mwetu kuelekeya kwenye Salaa ya ‘Iyd. Mtume (s.a.w) alikuwa akileta Takbira mpaka anamaliza Salaa.

[Silsilat Al Ahadiyth Swahiyhah -   Sheikh Al Albaaniy]

5)     Hakuna Hadiith inayohusiana na Rasuulullaah (s.a.w)  kwamba nini kisemwe wakati wa kuleta Takbira tunapoelekeya kusali, lakini Ibn Mas’uud alikuwa akisema yafuatayo:

Allaahu Akbar (mara mbili) (Mwenyezi Mungu ni Mkubwa)

Laa Ilaha Illallaaha (Hapana Mola Ila Mwenyezi Mungu)

Allaahu Akbar (mara mbili) (Mwenyezi Mungu ni Mkubwa)

Wa Lillaahil Hamdu (Na Shukrani Zote ni za Mwenyezi Mungu)

[Imesimuliwa na Ibn Abi Shaybah].

6)     Ni Sunnah kwa wenye kusali Salaa ya ‘Iyd kusali kwenye Musallah (katika uwanja ulio wazi) na sio Misikitini. Mtume (s.a.w) hakuwahi kusali Salaa ya ‘Iyd Msikitini. Abu Sa’iyd (r.a) amesimulia: “Mtume (s.a.w) alikuwa akienda kusali ‘Iyd-l-Fitr na ‘Iyd-l-Adh-haa kwenye Muswallaa, na kitu cha awali alichokuwa akikifanya ni kusali.” [Al Bukhaary na Muslim]

7)       Salaa ya ‘Iyd haina Adhana wala Iqaamah. [Muslim].

8)      Ibn ‘Abbaas amesimulia: “Mtume (s.a.w) Alisali rakaa mbili kwa ajili ya ‘Iyd na hakusali tena baada yake au kabla yake.” [Al Bukhaariy]

9)     Jabir (r.a) amehadithia: “ Mtume (s.a.w) alikuwa akirudi kutoka kwenye Salaa ya ‘Iyd-l-Fitr kupitia njia tofauti na ile aliyoendea.” [Al Bukhaariy].

10)    Siku ya Sikukuu inaruhusiwa kusikiliza nyimbo za Kiislaamu (Nashiyd, bila ya kutiwa ala za muziki) hususan kwa watoto. [Al Bukhaariy na Muslim]

Yaliyokuwa Bid’ah katika ‘Iyd

Ni Bid’ah (uzushi katika dini):

1)      Kunyoa ndevu hasa kwa makusudi ya kukusudia ‘Iyd. Mtume (s.a.w) ametukataza kunyoa ndevu zetu; ni aibu kufanya hivyo katika siku kubwa ambayo ni ya kufafanua na kudhihirisha tofauti ya sherehe zetu na zile za Mushrikin, Muislaam hunyoa ndevu akajisafisha kabisa na kuonekana kuwa hana tofauti (hufanana) na Mushrikin. 

2)     Kuwaiga Mushrikin katika mienendo yao na mavazi yao, na kupeana mikono na Wanawake. Mtume (s.a.w) amesema: “Ni bora kwa mwanamme kupigwa sindano katika kichwa chake kuliko kuushika mkono wa mwanamke ambaye si halali yake.”

       [Silsilat Al Ahadiyth Swahiyhah -   Sheikh Al Albaaniy] 

3)     Kusikiliza muziki siku ya ‘Iyd. Mtume (s.a.w) amesema: "Kutakuja watu katika umma wangu watakaozini, wanaume watakaovaa hariri, wengine watakunywa ulevi, na muziki utahalalishwa.” [Al Bukhaariy, Abu Dawuud na Al Bayhaqiy].

4)   Wanawake kutovaa vazi la stara (hijaab). Kufanya hivyo ni kusherehekea ‘Iyd na ilhali kunatendwa dhambi kubwa.

5)    Kuzuru makaburini hususan siku ya ‘Iyd. Inaruhusiwa kuzuru makaburini siku yoyote kwenye mwaka lakini isiwekwe kuwa siku ya ‘Iyd ni maalumu kufanya hivyo.

6)    Kuharibu pesa na kufanya israfu ya chakula badala ya kuwapa  maskini (na mafakiri).

Tunamuomba Allaah (s.w.t) Atusaidie tuepukane na Bid’ah, na Atuelekeze kwenye kuzifuata Sunnah za Mtume Wake (s.a.w).