TAWHIYD
    Tawhiyd

Qur'aan

Sunnah

Fiqhi

Makala

Nasiha Ya Ijumaa

Dua na Adhkaar

'Aqiyda-Tawhiyd

Vitabu

Darsa za Wanawake

    Sikiliza

Qur'aan

Mawaidha

Dua

Nashiyd

    Tizama

Video

 » Ramadhaan  

KUFUNGA SITA SHAWWAAL

Thawabu za kufunga sita Shawwaal hazipatikani ila baada ya kukamilisha mwezi wa Ramadhaan. Kwa hiyo kama mtu ana deni la Ramadhaan basi kwanza alipe deni kisha ndio afunge sita Shawwaal kwani Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kasema:

((من صام رمضان ثم أتبعه بست من شوال))

))Atakayefunga Ramadhaan, kisha akafuatia na Sita za Shawwal….((

[Muslim, Abu Dawud, Tirmidhi, Ibn Majah, Ahmad, ad-Daarimiy].

Kwa kutokana na Hadiythi hiyo tunasema kwamba,  yeyote mwenye deni la Ramadhaan alipe kwanza kisha ndio afunge Sita Shawwaal na ikiwa siku siku sita za Shawwaal zimeangukia siku ya Jumatatu na Alkhamiys atapata thawabu zote (thawabu za kufunga sita Shawwaal na thawabu za kufunga Jumatatu na Alkhamiys) kwa nia hizo kutokana na Hadiyth aliyosema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم

((إنماالأعمال بالنتات وإنما لكل امرئ ما نوى))

((Vitendo vinategemea (vinalipwa kwa) nia na kila mtu atapata kwa mujibu wa kile alichokusudia)).

Shaykh Muhammad bin Swaalih al-`Uthaymiyn Fiqhul Ibaadaat Ukurasa No.222 Maktabatul Iman